MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Serikali Yajizatiti Kukabiliana na Maafa – Majaliwa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Serikali Yajizatiti Kukabiliana na Maafa – Majaliwa
Habari

Serikali Yajizatiti Kukabiliana na Maafa – Majaliwa

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
MBEYA: WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imechukua hatua madhubuti kuimarisha ustahimilivu wa Taifa dhidi ya majanga kwa kutekeleza sera, sheria na miradi inayolenga kulinda maisha, mali na rasilimali za nchi.
Akizungumza jijini Mbeya katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kupunguza Madhara ya Maafa, Majaliwa amesema hatua hizo ni pamoja na kuhuisha Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Maafa (2025), Mkakati wa Taifa (2022–2027), na Mpango wa Kujiandaa na Kukabiliana na Maafa (2022).
Habari Picha 9953
Ameeleza kuwa Serikali imefanikiwa kuongeza usahihi wa utabiri wa hali ya hewa kupitia TMA hadi asilimia 85, hali ambayo imepunguza madhara ya maafa kwa zaidi ya asilimia 30. Pia, mifumo ya tahadhari ya mapema imeimarishwa kupitia teknolojia na Kituo cha Kitaifa cha Ufuatiliaji wa Majanga.
Katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, Waziri Mkuu amesema Serikali inatekeleza miradi mikubwa ya kimkakati kama vile ujenzi wa Bwawa la Kidunda (Tsh bilioni 329), Bwawa la Farkwa (Tsh bilioni 312), na Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria hadi Simiyu (Tsh bilioni 440).
Habari Picha 9954
Sekta ya kilimo pia imenufaika kupitia mbinu za kilimo himilivu kama umwagiliaji, matumizi ya mbegu bora, pamoja na mifumo ya tahadhari mapema ili kuwasaidia wakulima kukabiliana na majanga ya asili.
Waziri Mkuu amesema Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limeboreshwa kwa vifaa, teknolojia na mafunzo ya kisasa, jambo litakalowezesha uokozi wa haraka wakati wa majanga.
Ametoa wito kwa sekta binafsi kuwekeza kwenye miradi yenye mwelekeo wa ustahimilivu, ikiwemo uwekaji wa bima na kufuata miongozo ya serikali ili kuwalinda wananchi na mali zao.
Habari Picha 9955
Kwa upande wake, Waziri William Lukuvi na mwakilishi wa Umoja wa Mataifa, Sandra Hakim, wamehimiza ushiriki wa wadau wote katika usimamizi wa maafa, wakiwemo vijana, viongozi wa jamii, na taasisi za kimataifa katika kuzuia, kujiandaa na kurejesha hali baada ya majanga.

You Might Also Like

NIT yawapika vijana

Nzega Kujenga Barabara za Lami, Soko la Kisasa ili Kukuza Uchumi

Serikali Yajipanga Kuinua Maisha ya Vijana, Yaahidi Mabadiliko Kupitia Sera, Sheria

Viongozi Wa Dini Zote Wajifungie Kuomba,Kujadili Na Kutoa Mapendekezo-SAU

Ntonda Ameipongeza TEA Kwa Utekelezaji Bora Wa Miradi Ya Elimu

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article CHAUMMA Yataka Kuvunja Bodi ya Korosho, Kuunda Mamlaka Mpya ya Mazao ya Kimkakati
Next Article Wagonjwa 472 Waonwa Na Daktari Wa Mifupa MOI, 40 Wapendekezwa Kufika Dar kwa Matibabu
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vita Mashariki ya Kati Vyatikisa Uchumi wa SADC, Mawaziri Watakiwa Kuchukua Hatua
Habari March 12, 2026
Mamlaka Za Mitaa Ondoeni Urasimu Katika Kuanzisha Biashara Mpya-Waziri Mkuu
Habari March 12, 2026
Ofisi Ya Taifa Ya Takwimu  Kufanya Tafiti Kwa Wakala Wa Huduma Za Fedha,Viwandani
Habari March 12, 2026
GCLA  Yanunua Mitambo Mikubwa Inayogharimu Sh Bil 32.25 Kuimarisha Uchunguzi Wa Sampuli
Habari March 12, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?