MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Samia: Sera Iliyozinduliwa, Somo La Ujasiriamali Ni Lazima
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Samia: Sera Iliyozinduliwa, Somo La Ujasiriamali Ni Lazima
Habari

Samia: Sera Iliyozinduliwa, Somo La Ujasiriamali Ni Lazima

Author
By Author
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DODOMA: RAIS Samia Suluhu Hassan ameagiza kusimamiwa kikamilifu utekelezaji wa sera na Mitaala mipya ya elimu, ili ilete matokeo yaliyokusudiwa katika kuimarisha sekta ya elimu.
Rais Samia ametoa agizo hilo leo Februari mosi, 2025 wakati wa hafla ya uzinduzi wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya 2014 Toleo la mwaka 2023 iliyofanyika mkoani Dodoma.
Samia ameziagiza Wizara ya Fedha, Wizara ya Mipango na Uwekezaji. Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), kuwezesha kusimamia utekelezaji wa Sera na Mitaala hiyo mipya.
Amesema mabadiliko ya kukua kwa kasi kwa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ( TEHAMA), kunaweza kuwa mchango chanya au hasi kutokana na namna jamii itakavyojipanga.
“Ili kuendana na mabadiliko hayo ni lazima kutumia TEHAMA kutoa elimu kwa urahisi na kuwaandaa vijana wetu kuwa na taaluma na ujuzi wa taaluma zinazoendana na mageuzi ya TEHAMA bila kuathiri maadili ya vijana hao,” amesema.
Pia Rais Samia amesema serikali haina budi kuwa na maandalizi ya kutosha kwa kuinua viwango vya ubora wa elimu, kuwaandaa vijana vizuri zaidi ili wamudu stadi muhimu zitakazowawezesha kuajiriwa na kujiajiri, kuwajengea ujasiri na kuweza kujiamini.
Amesema dhamira ya kufanya mabadiliko katika Sera ni kumuandaa kijana anayejiamini na mwenye nyenzo stahiki za kukabiliana na ushindani wa kikanda na kimataifa ili kutumia utajiri wa rasilimali za nchi, anufaike kiuchumi.
“Sera iliyoboreshwa pia italeta somo la ujasiriamali ambalo litakuwa la lazima kwa kila mwanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha nne ili kumuandaa mwanafunzi kupata misingi ya biashara,” amesema.
Amesema ili mwanafunzi huyo akiamua kujiajiri kwa kutumia stadi alizopata shuleni, aweze kufanya shughuli zake akiwa na maarifa ya biashara na apate manufaa zaidi.

You Might Also Like

Maboresho sheria, kanuni za madini yameongeza mapato

Ongezeni Uwajibikaji,Nidhamu, Utendaji Kazi – Bashungwa

Masoko mapya nje ya nchi kuipatia nchi sh. trilioni 10

Rais Samia Azindua Makao Makuu Ya Mahakama Tanzania

RC Chalamila, Wasaidizi Wake Kukutana na Kadogosa Kuzungumzia Ujenzi Wa Reli Dar

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TEA Kuhakikisha Mazingira Ya Kujifunzia, Kufundishia Yanaboreshwa
Next Article Askari Wawili wa JWTZ Wafariki, Wanne Wajeruhiwa DRC
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?