MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Samia Mgeni Rasmi Siku Ya Wanawake Jijini Arusha
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Samia Mgeni Rasmi Siku Ya Wanawake Jijini Arusha
Habari

Samia Mgeni Rasmi Siku Ya Wanawake Jijini Arusha

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: RAIS Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kitakachofanyika mkoani Arusha.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima amesema hayo alipozungumza na Waandishi wa Habari kuhusu uelekeo wa maadhimisho hayo.
Gwajima amesema kama taifa linayo mengi ya kujivunia ambayo ni kielelezo  cha utashi na uthubutu wa Rais Samia katika kukuza usawa na uwezeshaji wanawake nchini.
” Serikali kwa kutambua umuhimu wa siku hii inahimiza wanawake na wananchi kwa ujumla kujitokeza katika maadhimisho kwa kushiriki matukio yote kuanzia uzinduzi, maonesho na makongamano ili kuwa na maadhimisho yenye tija na mafanikio kwa ustawi na maendeleo ya wanawake hapa nchini,” amesema.
Amesema kauli ya mwaka huu ni  ‘Wanawake na Wasichana 2025’ inalenga kuhamasisha jamii katika kukuza usawa, haki na uwezeshaji wa wanawake na wasichana na kwa kuzingatia kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
Amesema lengo la kaulimbiu ni kuwafanya wanawake na wasichana wajiamini, wajiandae na wajitokeze kugombea fursa za uongozi.
Amesema katika kuadhimisha siku hii, serikali imeunda kamati ya Kitaifa ya maandalizi ya maadhimisho hayo kwa lengo la kuhakikisha yanabeba sura ya kitaifa na kushirikisha wadau wote.
Amesema Machi mosi, 2025 uzinduzi utafanyika katika mikoa, wilaya na Kata zote nchini.
Machi tatu hadi sita mwaka huu 2025, kutafanyika makongamano ya Kikanda katika mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Dodoma, Geita, Mbeya, Lindi na Kigoma.
Amesema Machi tano mpaka nane, 2025 kutakuwa na maonesho ya wanawake wajasiriamali, taasisi za umma na binafsi na makampuni jijini Arusha.
Na Machi nane, mwaka huu itakuwa kikele cha maadhimisho hayo.

You Might Also Like

UDOM Yatafiti Dawa za Malaria, Vidonda vya Tumbo, Kisukari Kutoka Mimea ya Asili

Jeshi la polisi kuchukua tahadhari mechi ya Simba, Yanga leo

Wafanyabiashara: Tupo Tayari Kushirikiana na Serikali

Kafulila: Ushirikiano wa Sekta Binafsi na Umma Kuboresha Huduma

VETA Yaleta Mapinduzi ya Kilimo na Biashara Kupitia Bunifu –  Profesa Nombo

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Matwebe Aipongeza Serikali Kushirikisha JUMIKITA  Kwenye Shughuli Za Kitaifa
Next Article Italia Kuangazia Fursa Za Uwekezaji Ambazo Hazijatambuliwa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Bunge Marathon kufanyika April 18,yakidhi viwango vya kimataifa
Habari April 14, 2026
Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu, Aongoza Harambee Mei Mosi 2026
Habari April 14, 2026
Ubunifu Wa Majengo Watakiwa Kuzingatia Tija Na Gharama Nafuu
Habari April 11, 2026
Waziri Ulega aridhishwa na miradi ya dharura TANROADS
Habari April 11, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?