MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Rais CWT Asikitishwa Na Uzembe, Maofisa Wa Halmashauri
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Rais CWT Asikitishwa Na Uzembe, Maofisa Wa Halmashauri
Habari

Rais CWT Asikitishwa Na Uzembe, Maofisa Wa Halmashauri

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read

Asisitiza Kuendeleza Safari ya Tumaini kwa Walimu

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: RAIS wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Mwalimu Suleiman Ikomba, ameeleza kusononeshwa na baadhi ya Maofisa wa Halmashauri kushindwa kutekeleza wajibu wao kwa ufanisi, licha ya serikali kuu kutoa maelekezo ya wazi juu ya maslahi ya walimu.

Ameeleza hayo alipozungumza na Mwandishi wa habari hii alipotaka kujua ni nini kinachomsononesha kuhusu waalimu hapa nchini.

Amesema moja ya mambo yaliyomvunjia moyo katika safari yake ya uongozi ni kukutana na walimu waliopaswa kupandishwa madaraja kwa mujibu wa sifa zao, lakini wakaachwa kwa sababu ya uzembe wa maofisa wa utumishi katika ngazi ya halmashauri.

“Tumeona walimu waliokuwa na sifa sawa, waliopaswa kupanda madaraja pamoja, lakini mmoja anapandishwa na mwingine anaachwa.

“Wengine wanazidiwa mshahara kwa zaidi ya laki mbili ilhali wameajiriwa siku moja, wana elimu sawa, na wanatekeleza majukumu sawa. Hali hii ni ya kusikitisha na inawaumiza walimu,” amesema.

Amesema uzembe huo unaofanywa na baadhi ya maofisa ni chanzo kikuu cha malalamiko yasiyopaswa kuwepo, hasa ikizingatiwa kuwa serikali kuu imeonyesha nia thabiti ya kutatua changamoto za walimu kupitia maagizo rasmi yanayopaswa kufanyiwa kazi kwenye halmashauri.

“Maagizo kutoka serikali kuu yalikuwa wazi. Tukiwa pamoja na viongozi wa serikali tulitembelea mkoa kwa mkoa, tukakutana na walimu, tukapokea malalamiko yao. Cha kusikitisha ni kuona baadhi ya halmashauri wakishindwa kutekeleza maagizo hayo. Huu ni uzembe wa mtu mmoja lakini unagharimu maisha ya wengi,” amesema.

Kwa upande mwingine ameelezea kufurahishwa na namna ambayo serikali imekuwa ikishirikiana na CWT katika kuzishughulikia kero za walimu.

“Jambo lililonipa furaha isiyoelezeka ni namna tulivyotembea na serikali mkoa kwa mkoa kupitia kliniki ya walimu, tukisikiliza kero zao, tukitafuta suluhu. Kupokelewa na wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, walimu wakifunguka matatizo yao moja kwa moja hiyo ilikuwa safari ya matumaini,” amesema.

Ameahidi katika kipindi chake cha uongozi wa miaka mitano kutoka mwaka huu 2025 hadi 2030, kwamba atahakikisha CWT inabaki kuwa sauti ya kweli ya walimu wote.

Amesema anataka kuwa kiongozi mtetezi wa haki katika kiwango cha ubora unaostahili.

“Natamani kuwa mtetezi wa walimu, lakini kwa njia inayolinda hadhi ya taaluma yetu. Nimegombea kwa sababu nimeona kuwa kazi nzuri imeanza kufanyika.

“Niko hapa kuwahudumia kwa ukamilifu, na kuhakikisha kazi yetu ya ualimu inabaki kuwa yenye heshima na tija kwa taifa,” amesema.

You Might Also Like

Stamico Yahimiza Ubunifu, Uaminifu Na Kujituma

‘Upungufu wa Wakunga Afrika Watishia Maisha ya Mama na Mtoto ‘TAMA

Samia Mgeni Rasmi Siku Ya Wanawake Jijini Arusha

Wakulima wafunzwa kuhusu mlipuko wa panya TPHPA

Serikali Yaendelea Kuimarisha Uhuru wa Mahakama – Nchimbi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Rais Mpya CWT Ikomba: ‘Nataka Kuwaunganisha Walimu, Kuitendea Haki Kazi Yetu’
Next Article Samia Aleta Mapinduzi Arusha
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Serikali Yaingia Makubaliano Ya Ushirikiano Na DIT Kuimarisha Usimamizi Wa Mataifa
Habari June 8, 2026
Wananchi Waelimishwa Masharti ya Kubadilisha Noti Zilizochakaa, Kuungua na Kuchanika
Habari June 7, 2026
DMI Yawaalika Vijana Kujiunga Na Masomo Ya Ubaharia
Habari June 6, 2026
Taifa Gas Yaendelea Kuongoza Kampeni ya Nishati Safi kwa Taasisi na Sekta ya Utalii Tanzania
Habari June 6, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?