MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Profesa Nagu Aridhishwa Na Huduma Katika Banda Jumuishi La Ofisi Ya Waziri Mkuu Sabasaba 
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Profesa Nagu Aridhishwa Na Huduma Katika Banda Jumuishi La Ofisi Ya Waziri Mkuu Sabasaba 
Habari

Profesa Nagu Aridhishwa Na Huduma Katika Banda Jumuishi La Ofisi Ya Waziri Mkuu Sabasaba 

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Lucy Lyatuu
NAIBU  Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya katika Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Profesa Tumaini Nagu, ametembelea Banda Jumuishi la Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi zake katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba 2026) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam, na kupongeza ubora wa huduma zinazotolewa kwa wananchi.
Akiwa katika ziara hiyo, Profesa Nagu amepata fursa ya kutembelea sehemu mbalimbali za banda hilo na kupokea maelezo kuhusu huduma na mifumo mbalimbali inayowezesha wananchi kupata taarifa na huduma zinazotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na taasisi zake.
Amesema banda hilo limekuwa jukwaa muhimu la kuwaelimisha wananchi kuhusu utekelezaji wa programu na miradi ya maendeleo inayolenga kuboresha utoaji wa huduma za kijamii, hususan katika sekta ya afya, elimu, utawala bora na maendeleo ya serikali za mitaa.
Habari Picha 12800
Profesa Nagu amewapongeza watumishi wanaohudumu katika banda hilo kwa kujituma, kutoa elimu kwa ufasaha na kuhakikisha kila mwananchi anayefika anapata huduma na taarifa sahihi zinazomwezesha kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu.
Aidha, amewataka kuendelea kutumia maonesho hayo kama fursa ya kusikiliza maoni ya wananchi, kupokea changamoto zao na kutoa ufafanuzi wa kina kuhusu huduma zinazotolewa, ili kuongeza uelewa na kuimarisha uhusiano kati ya Serikali na wananchi.
Habari Picha 128018
“Banda Jumuishi la Ofisi ya Waziri Mkuu limeendelea kuvutia maelfu ya wananchi wanaotembelea Maonesho ya Sabasaba, ambapo wamekuwa wakipata elimu na huduma mbalimbali zinazotolewa na Ofisi hii pamoja na taasisi zake kwa lengo la kuboresha ustawi wa wananchi na kuharakisha maendeleo ya Taifa, hivyo wananchi endeleeni kuitumia fursa ya uwepo wa ofisi hii katika maonesho haya,” amesema Dkt. Nagu
Habari Picha 12802
Habari Picha 12803

You Might Also Like

Tanzania Na Namibia Kuongeza Juhudi Kukuza Ushirikiano Wa Kiuchumi

Ridhiwani: WCF Umeboresha Mifumo Ya Ushughulikiaji Wa Fidia

Waziri Mkuu Majaliwa Kuongoza Harambee Ya Mei Mosi Kitaifa

Dendego Achangisha Bilioni 1.7, Ujenzi Ofisi Ya CCM

Tume ya Kurekebisha Sheria Yatoa Onyo Kali kwa Wanaovunja Sheria za Umwagiliaji

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article JAB Yazindua Mwongozo Wa Kisheria Wa Utoaji Ithibati Ya Maisha Kwa Wanahabari Wakongwe
Next Article Misitu Ni Moyo Wa Maendeleo Endelevu-TFS
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mfuko Wa Utamaduni Watoa Sh Bil 14.7 Kwa Miradi Ya Sanaa
Habari August 26, 2026
BMT Kutumia Tamasha La Taifa La  Utamaduni Kuelimisha Wananchi Kuhusu Fursa Za Afcon
Habari August 26, 2026
Teknolojia Ya SmartShamba Planter Yageuza Dakika 30 Kuwa Tumaini La Mkulima
Makala August 25, 2026
OUT: Elimu Sasa Kiganjani
Habari Uncategorized August 24, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?