MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Profesa Laizer Kupambana Na Umaskini, Ujinga, Maradhi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Profesa Laizer Kupambana Na Umaskini, Ujinga, Maradhi
Habari

Profesa Laizer Kupambana Na Umaskini, Ujinga, Maradhi

Author
By Author
Share
3 Min Read
– Dkt. Ikomba Aahidi Kutumikia Taifa Kwa Moyo Wa Uzalendo Na Kujitolea
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: PROFESA mteule Julius Laizer ametunukiwa uprofesa wa heshima na Chuo cha In His Name Bible College (IHNBC) cha Marekani, na kuahidi kutumia heshima hiyo kupambana na changamoto kuu zinazokwamisha maendeleo ya Watanzania ikiwemo ujinga, umaskini na maradhi.
Habari Picha 9405
Amesema hayo katika mahafali ya pili ya chuo hicho yaliyofanyika katika Kanisa la Baptist, Kinondoni B jijini Dar es Salaam.
Amesema atatumia ndoto hiyo kupambana na hao maadui watatu.
“Laizer amesema kutunukiwa uprofesa wa heshima ni kutimia kwa ndoto yake ya utotoni.
“Tangu nikiwa na umri wa chini ya miaka nane nilitamani kusoma na kuwa mtu mkubwa. Leo hii, ndoto hiyo imetimia,” amesema Profesa Laizer.
Amesisitiza kuwa amani ni msingi wa maendeleo ya nchi yoyote na kuitaka jamii kuihifadhi kwa nguvu zote.
“Dumisheni amani Tanzania, maana amani ni bora kuliko vitu vyote. Amani ikiwepo, haki hutendeka,” amesema.
Amewahimiza Watanzania kufanya kazi kwa bidii, kuwa wabunifu na kutumia elimu kama silaha ya kupambana na umasikini na ujinga, akiongeza kuwa maendeleo yanahitaji juhudi za pamoja.
Habari Picha 9407
Katika mahafali hayo, wahitimu 21 walitunukiwa vyeti mbalimbali, watatu walipewa diploma ya theolojia, watano shahada ya kwanza ya theolojia, 12 walitunukiwa Shahada ya Uzamivu ya Heshima akiwemo Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Dkt. Suleiman Ikomba,
Na mmoja Julius Laizer alitunukiwa uprofesa wa heshima kwa mwaka wa masomo 2024/2025.
Miongoni mwa waliotunukiwa Shahada ya Uzamivu ya Heshima yumo Mchungaji Jonathan Mtibona wa Kanisa la EAGT Ilemela, Mwanza, ambaye amesema heshima hiyo ni ishara ya kutambuliwa kwa kazi yake ya utumishi kwa jamii na kanisa.
Habari Picha 9408
“Nimeweza kusimamia ujenzi wa makanisa katika mikoa ya Kigoma na Mwanza yenye thamani ya zaidi ya Sh.Bilioni 2. Pia ni mwalimu wa uchumi na mwanzilishi wa shule ya awali kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu inayojulikana kama Maisha Mapya Charity,” amesema Mtibona.
Naye Dkt. Arnold Manase aliyepokea shahada hiyo ya heshima katika fani ya Uongozi na Ushauri Nasaha, amesema shahada hiyo ni kichocheo cha kutumia uwezo wake kikamilifu kwa ajili ya kusaidia jamii.
Rais wa CWT, Dkt. Ikomba, ameeleza kuwa heshima hiyo imempa nguvu na chachu ya kuendelea kulitumikia taifa kwa moyo wa uzalendo na kujitolea.
Habari Picha 9406
Chuo cha In His Name Bible College kimeendelea kutoa heshima kwa viongozi wa dini na jamii wanaochangia maendeleo kupitia huduma za kiroho, kijamii na kielimu, ikiwa ni njia ya kuwatambua na kuwahamasisha kuendelea na kazi zao za kiutumishi kwa jamii.

You Might Also Like

Mtindi wa Korosho, Stafeli Wafanyiwa Utafiti UDSM

Matokeo Ya Usaili TRA Kutangazwa April 25,2025

Vyuo vya Kilimo vishirikishwe mradi wa BBT

Tanzania Ina Utolevu Wa Chakula Kwa Miaka Minne Uongozi Wa Samia

Bodi ya Bima ya Amana Yatoa  Bil 9.07 , Fidia Kwa Wateja Wa Benki Saba   Zilizofilisika

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article CHAUMMA Kuunda Mamlaka ya Mazao ya Kimkakati – Salum Mwalim
Next Article Wananchi Watakiwa Kufahamu Sheria Na Miongozo
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Waziri Mkuu Majaliwa Akabidhi Tuzo kwa BoT Geita
Habari September 22, 2025
BoT Yarahisisha Uuzaji wa Dhahabu kwa Wachimbaji, Yatoa Punguzo La Mrabaha
Habari September 22, 2025
Waziri Mkuu Apongeza Huduma Kidijitali za NSSF, Maonesho Ya Madini Geita
Habari September 22, 2025
Mkuu Wa Mkoa Shinyanga Asifu Kazi Ya Bodi Bima Ya Amana
Habari September 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?