MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wananchi Watakiwa Kufahamu Sheria Na Miongozo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wananchi Watakiwa Kufahamu Sheria Na Miongozo
Habari

Wananchi Watakiwa Kufahamu Sheria Na Miongozo

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Mwandishi Wetu
DODOMA: WANANCHI wametakiwa kutambua kuwa Katiba ya Tanzania hubeba masharti ya jumla kuhusu masuala mbalimbali ya nchi, lakini ufafanuzi wa kina hupatikana kupitia sheria, kanuni na miongozo mingine rasmi.
Mwandishi Mkuu wa Sheria nchini, Onorius Njole, ameeleza hayo alipowasilisha mada kuhusu majukumu na mafanikio ya Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria (OCPD), katika kikao kazi kati ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari, kilichofanyika jijini Dodoma.
Njole amesema baadhi ya malalamiko ya wananchi juu ya kunyimwa haki zao yanatokana na kutotambua kuwa Katiba haitoi haki hizo moja kwa moja bali huweka msingi wake, ambao unahitaji kusomwa sambamba na sheria husika.
Habari Picha 9414
Ametoa mfano wa haki ya kuishi iliyo kwenye Katiba, lakini sheria inaruhusu adhabu ya kifo kwa makosa ya jinai maalum.
Ameongeza kuwa haki ya kuchagua na kuchaguliwa, ambayo pia imo kwenye Katiba, hutekelezwa kwa kuzingatia sheria na miongozo ya Tume ya Uchaguzi.
“Ukifika kupiga kura saa mbili usiku, huwezi kusimama na Katiba kudai haki yako  kuna utaratibu unaopaswa kuzingatiwa.” amesema.
Kwa msingi huo, amewataka wahariri na wanahabari kusaidia jamii kuelewa namna Katiba, sheria, na miongozo vinavyofanya kazi kwa pamoja ili kupunguza upotoshaji na sintofahamu kuhusu masuala ya kisheria.
Akielezea mafanikio ya Ofisi hiyo kwa kipindi cha miaka mitano,  Njole amesema kuwa ofisi yake imekamilisha kazi ya urekebishaji wa sheria na kuchapisha Toleo la Mwaka 2023, kutafsiri sheria kuu 433 kati ya 446 kwa Kiswahili, na kufanya upekuzi wa mikataba 3,446 pamoja na hati za makubaliano 729.
Pia wameandaa sheria 68 na kutengeneza sheria ndogo 5,708.
Ameahidi ofisi yake itaendelea kushirikiana kwa karibu na wanahabari katika kutoa ufafanuzi wa masuala ya kisheria ili kujenga uelewa wa pamoja na kusaidia taifa kufikia maendeleo kupitia utawala bora wa sheria.
Awali, akifungua kikao kazi hicho, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali,  Samweli Maneno amewataka wahariri kuhakikisha habari zinazohusu sheria zinatoka kwa mamlaka sahihi ili kuepusha upotoshaji wenye athari kwa taifa na jamii.
Maneno amesisitiza kuwa amani na umoja vinavyotokana na utawala wa sheria ni msingi wa utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2020.
Amesema pasipo amani, hakuna shughuli ya maendeleo itakayoweza kufanyika, hivyo ni muhimu kuzingatia haki, wajibu, na sheria zinazotuongoza.

You Might Also Like

Rais Samia akisikiliza jambo

Katambi Awataka CBE Kutoa Elimu Yenye Ushindani Kimataifa

VETA kushirikiana na Toyota Tanzania kuboresha mafunzo ya ufundi magari

Heshima ya Udaktari Ni Mwito wa Kulitumikia Taifa: Dkt Ikomba

Wafanyabiashara 45 Wa Tanzania Wameanza Kutumia Soko La Eneo Huru La Afrika

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Profesa Laizer Kupambana Na Umaskini, Ujinga, Maradhi
Next Article MOI Yazindua Mfumo Mpya Wa Kielektroniki Wa Kupanga Miadi Na Madaktari
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mradi Wa Umeme Mpomvu-GGM Kuimarisha Upatikanaji Wa Umeme Na Kuchochea Shughuli Za Kiuchumi Geita- Salome
Habari September 4, 2026
Wahitimu 794 Wa Vyuo Vya Elimu Ya Juu Waomba Kujiunga VETA
Habari September 4, 2026
Taka za saluni zageuka dhahabu ya kijani: COSTECH yamulika safari ya David kutoka wazo hadi hataza
Makala September 4, 2026
Umeme Kubadilisha Maisha Ya Wakazi Wa Kisiwa Cha Jibondo Mafia
Habari September 3, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?