MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: NSSF Kutekeleza Mradi Wa Uwekezaji Wa Jengo La Kitega Uchumi Dodoma
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > NSSF Kutekeleza Mradi Wa Uwekezaji Wa Jengo La Kitega Uchumi Dodoma
Habari

NSSF Kutekeleza Mradi Wa Uwekezaji Wa Jengo La Kitega Uchumi Dodoma

Author
By Author
Share
5 Min Read

Na Mwandishi Wetu
MFUKo wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), unatarajia kufanya uwekezaji mkubwa katika Jiji la Dodoma kwa kujenga jengo la minara miwili ambalo litachochea ukuaji wa uchumi na utalii katika jiji hilo.

Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba amesema hayo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea mradi huo pamoja na zoezi la kupanda miti katika kiwanja namba 3 kitalu F, kilichopo Njedengwa jijini Dodoma.

Mshomba amesema NSSF imeamua kuwekeza katika mradi huo kwa sababu shughuli za uwekezaji ni jambo la msingi na wamekuwa wakiwekeza kwenye maeneo tofauti tofauti .Amesema lengo la kuwekeza ni ili kuhakikisha thamani ya michango ya wanachama haipotei na kupata faida inayoiwezesha Mfuko kulipa mafao kwa wanachama wake.

Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Moshomba amesema utekelezaji wa ujenzi wa mradi huo unatarajiwa kuanza Mei 2025 na utakamilika ndani ya kipindi cha miaka mitatu.

Amesema miongoni mwa faida zinazotarajiwa kupitia mradi huo ni kuchochea utalii wa mikutano, kuvutia wawekezaji na kuongeza ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja. Mradi huo unatarajiwa kugharimu sh bilioni 148.40 kwa gharama za awali za mradi.

Mshomba amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa juhudi ambazo amekuwa akizifanya katika kuboresha mazingira ya uwekezaji nchini, ambapo kwa upande wa NSSF imepata mafanikio makubwa katika miaka ya hivi karibuni kwa kuongeza wanachama na waajiri pamoja na ongezeko la michango na kusababisha thamani ya Mfuko kufikia trilioni 8.5.

“Mafanikio yote hayo yanatokana na juhudi kubwa ambazo Mheshimiwa Rais wetu amezifanya katika kuboresha mazingira ya uwekezaji, lakini pia juhudi zinazochukuliwa na Bodi ya Wadhamini, Ofisi ya Waziri Mkuu na BoT,” amesema Mshomba.

Amesema Juni 2024, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alipofanya ziara ya kikazi katika jiji la Mwanza alitembelea mradi wa uwekezaji wa jengo la hoteli ya nyota tano ambapo alishauri NSSF ikipata mapato mazuri zaidi, uiangalie kuwekeza kwenye maeneo mengine ikiwemo mji wa kiserikali Dodoma, hivyo pamoja na kutekeleza mpango wa NSSF kuwekeza Dodoma kwa mujibu wa miongozo na sera za uwekezaji lakini pia ni utekezaji wa maono na maelekezo ya Rais.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule ameipongeza NSSF kwa mpango wa utekelezaji wa ujenzi wa mradi huo mkubwa ambao utachochea ukuaji wa uchumi na utalii katika mkoa huo ambao ndio Makao Makuu ya Nchi, utaleta heshima katika Kanda ya Kati na Taifa kwa ujumla.

Rosemary amesema Serikali inaendelea kutekeleza mikakati mbalimbali yenye malengo ya kukuza uchumi pamoja na biashara ya utalii na kuwa mikakati hiyo imeanza kuzaa matunda baada ya RaisDkt. Samia Suluhu Hassan kuifungua nchi pamoja na kuzindua filamu ya ‘The Royal Tour’ ambayo imechangia ongezeko kubwa la watalii.

Amesema ujenzi wa kitega uchumi hicho cha NSSF utakuwa chachu ya kuchochea uchumi.

“Mimi ninaposhuhudia NSSF mnakuja kuwekeza mradi mkubwa wa namna hii nawaona ni waelewa wa haraka sana wa kumuelewa Mhe. Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan,” amesema Rosemary.

Amesema mojawapo ya vitu ambavyo Rais anatamani kuviona ni Mkoa wa Dodoma ambao ndio Makao Makuu ya Nchi kuleta mikutano ya kimataifa, hivyo ujenzi wa jengo hilo la kitega uchumi la NSSF linaendana na azma ya Serikali ya awamu ya sita ambayo inaendelea kuufungua mkoa huo pamoja na maeneo mengine nchini.

Rosemary amesema kukamilika kwa hoteli hiyo pamoja na uwanja wa ndege wa Msalato utachochea shughuli za kiuchumi, kufungua fursa mpya za mikutano ya kimataifa jijini humo, kuongeza mnyororo wa thamani pamoja na kuzalisha ajira.

Ametumia fursa hiyo kuipongeza NSSF kwa kupata mafanikio mbalimbali ambapo hivi sasa thamani ya Mfuko imefikia trilioni 8.5 jambo ambalo limechangiwa na kuwepo kwa ongezeko kubwa la wawekezaji, kukua kwa sekta binafsi na kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi.

Awali, akitoa taarifa ya mradi huo, Meneja Usimamizi Wa Miradi NSSF Helmes Pantaleo, amesema mradi huo unatarajiwa kujengwa jengo la ghorofa 16 na kuwa umegawanyika sehemu tatu ikiwemo ya ofisi, hoteli na maduka makubwa.

Amesema hoteli hiyo itakuwa na vyumba 120 kikiwemo chenye hadhi ya kulala viongozi wakuu na migahawa mbalimbali.

You Might Also Like

Majaliwa  awataka waandamizi, vyombo vya usalama kutekeleza 4R

Ridhiwani Awashika Mkono Wenye Mahitaji Maalum

Ndege Ya TPHPA Yatua Rasmi Kudhibiti, Kwelea Kwelea, Viwavijeshi, Nzige 

TRA: Serikali imemgusa mkulima kupitia mabadiliko ya sheria

Zuhura Yunus Atoa Neno Kwa Madereva 

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TALGWU Chafanya Kikao Cha Baraza La Wafanyakazi Dodoma
Next Article Polisi Kuimarisha Ulinzi Nyumba Za Ibada Krismasi, Mwaka Mpya
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?