MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Njaa, Mafao Ya Wakulima Vyatikisa Kampeni Za Ubunge Dodoma Mjini
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Njaa, Mafao Ya Wakulima Vyatikisa Kampeni Za Ubunge Dodoma Mjini
Habari

Njaa, Mafao Ya Wakulima Vyatikisa Kampeni Za Ubunge Dodoma Mjini

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Danson Kaijage
DODOMA: MGOMBEA UQbunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Jimbo la Dodoma Mjini, Fatuma Waziri, amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuulizwa maswali na wanachama wa chama chake wakati wa mkutano wa kampeni katika Kata ya Mpunguzi.
Mmoja wa wajumbe wa CCM kata ya Mpunguzi, Josefu Mhawi, amemuuliza mgombea huyo kuhusu hatma ya wakulima wanapozeeka, ikilinganishwa na wafanyakazi wa kawaida wanaopata mafao yao baada ya kustaafu.
“Tanzania ina watu wawili: wakulima na wafanyakazi. Mfanyakazi anapostaafu analipwa pensheni yake. Mkulima anapozeeka halipwi chochote.
“Je, endapo utachaguliwa kuwa mbunge, utatuteteaje wakulima ili na sisi tulipwe mafao, kwani tumetumia muda wetu kulilisha taifa?” alihoji Mhawi,”amehoji.
Maswali hayo yaliibua mjadala mzito na kumweka mgombea katika hali ya sintofahamu kwa muda, hata akasahau jina la Kata aliyopo.
Kwa upande wake Mjumbe wa CCM katika Kata hiyo,  Paulo Lyasweye,  amehoji kuhusu namna mgombea huyo atakavyosaidia wananchi kupata mahindi ya msaada na kusema ukweli bungeni kuhusu hali halisi ya mfumuko wa njaa nchini.
“Kumekuwepo na tatizo la njaa kutokana na ukame, lakini viongozi wamekuwa wakilificha suala hili. Wakati mwingine mahindi ya msaada huuuzwa kwa bei ya juu. Je, wewe ukiwa mbunge, utatusaidiaje kupaza sauti bungeni na kupunguza bei ya mahindi ya msaada?” amehoji Lyasweye.
Akijibu maswali hayo, Fatuma amesema iwapo atachaguliwa, atakutana na wananchi kujadiliana jinsi ya kupeleka mapendekezo bungeni ili kuangalia uwezekano wa wakulima kunufaika na mfumo wa mafao.
Kuhusu suala la chakula cha msaada, amesema analiona kama hitaji la msingi linalopaswa kuwekewa mkazo kwa kubadili sera na kuondoa ubabaishaji uliopo sasa.
Wagombea wengine waliojitokeza kuwania nafasi hiyo ya ubunge walikuwa ni Mhandisi Rashid Mashaka, Pascal Inyasi Chinyele, Samwel Marwa Kisaro, Robert Daniel Mwinje, Rosemary Chabe Jairo na Abdulhabib Jafar Mwanyemba. Kwa pamoja, walitoa ahadi za kupeleka huduma ya maji, kuboresha afya, elimu na ustawi wa wananchi wa Dodoma Mjini.

You Might Also Like

Tutuba: Noti Mpya Kuanza Kutumika Februari Mosi mwaka huu

TARI yapongezwa kwa kuwa na teknolojia bora za kilimo

Ushirikiano Wanataalum, Wanatasnia Kisekta Ni Muhimu Katika Maendeleo Kiuchumi

Waajiri Wasilisheni Michango Kwa Wakati

Msigwa Azikumbusha Taassisi Za Serikali, TANROAD Ikielezea Mafanikio Yake

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Asha Moto Aibuka Kidedea Ubunge wa Viti Maalum Mtwara Kupitia CCM
Next Article Malecela: Nitakuza Vipaji, Nitafutia Vijana Ajira Dodoma Mjini
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Waziri Mkuu Majaliwa Akabidhi Tuzo kwa BoT Geita
Habari September 22, 2025
BoT Yarahisisha Uuzaji wa Dhahabu kwa Wachimbaji, Yatoa Punguzo La Mrabaha
Habari September 22, 2025
Waziri Mkuu Apongeza Huduma Kidijitali za NSSF, Maonesho Ya Madini Geita
Habari September 22, 2025
Mkuu Wa Mkoa Shinyanga Asifu Kazi Ya Bodi Bima Ya Amana
Habari September 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?