MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mwalim: Nitarudisha Hadhi ya Dar es Salaam Kama Jiji Kamili
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mwalim: Nitarudisha Hadhi ya Dar es Salaam Kama Jiji Kamili
Habari

Mwalim: Nitarudisha Hadhi ya Dar es Salaam Kama Jiji Kamili

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
MGOMBEA wa urais kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalim, ameahidi kuirejeshea Jiji la Dar es Salaam hadhi yake ya awali endapo atachaguliwa kuwa Rais.
Akihutubia wakazi wa Dar es Salaam katika moja ya mikutano ya kampeni, Mwalim amesema kuwa Dar es Salaam ni kitovu cha biashara na uchumi nchini, hivyo inastahili kuwa na Meya wa Jiji mwenye mamlaka kamili ya kisheria na kiutendaji.
“Nitairudishia Dar es Salaam heshima yake ya kuwa Jiji kamili, lenye Meya wa kuchaguliwa atakayewajibika kwa wananchi. Jiji hili linaingiza mapato makubwa serikalini, hivyo linastahili kuheshimiwa,” amesema.
Habari Picha 9923
Pamoja na hilo, ameeeleza dhamira yake ya kuboresha maisha ya watumishi wa umma kwa kuongeza kima cha chini cha mshahara hadi Sh. Milioni nane ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuinua uchumi wa familia na kupunguza utegemezi.
 “Naombeni mniamini na kunipa nafasi hii. Nina nia ya kweli ya kubadili maisha ya Watanzania. Vijana wapate ajira stahiki — maana kubeti si kazi,” amesema.
Katika mkutano huo huo, Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kinondoni kupitia CHAUMMA, Moza Ally, amewataka wananchi wa jimbo hilo kumchagua kwa msingi wa utendaji usio na ubaguzi.
“Baada ya kuapishwa, sitakuwa mbunge wa mfukoni. Nitakuwa mbunge wa wananchi wote. Wale waliokata tamaa waamini tena kuwa kuna matumaini,” amesema.
Moza ameahidi kuwa ofisi ya mbunge itakuwa wazi kwa wananchi wa vyama vyote na kusimamia upatikanaji wa mikopo ya maendeleo, hususani kwa vijana na wanawake, ambayo amedai kwa muda mrefu imekuwa changamoto.
“Kila mwananchi atahudumiwa bila kujali itikadi ya kisiasa. Ile mikopo mliyokuwa mkiikosa, sasa mtaipata,” amesema.
Wagombea hao wamekuwa wakihimiza siasa za heshima na kujikita katika sera zenye kuangazia maendeleo na ustawi wa wananchi, wakitumia kaulimbiu ya mabadiliko ya kweli.

You Might Also Like

Tulia Atoa Taarifa Kifo Cha Ndugai

Wanafunzi Shule Ya Anlex, Walimu Wao Watinga Bungeni

Kabonaki: Jiungeni Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Hiari

Kiwanda cha Sukari Mkulazi Chaanza Kuleta Tija, Sangu Apongeza Uwekezaji wa NSSF na Magereza

TEA, Wadau Kuwezesha Matumizi Safi Nishati Ya Kupikia Mashuleni

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Serikali Yajipanga Kuinua Maisha ya Vijana, Yaahidi Mabadiliko Kupitia Sera, Sheria
Next Article Profesa Ndunguru: Teknolojia ya Vinasaba Yafungua Ukurasa Mpya Katika Kilimo
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

VETA kumpa nafasi Igobeko kuongeza ujuzi na kuwawezesha wengine
Habari August 23, 2026
Airtel Yajenga Darasa La Fursa Katika Shule Ya Sekondari Magaoni,Tanga
Habari August 23, 2026
Bunifu ya dawa ya mayai yapunguza hasara kwa wafugaji wa kuku
Makala August 22, 2026
Dkt Yonaz Awakumbusha Vijana Kulinda Afya Zao Katika Mapambano Dhidi Ya Ukimwi
Habari August 22, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?