MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mkuu Wa Wilaya Komba Aitaka DIB Kuongeza Ulinzi Kwa Fedha Za Wananchi Katika Vikoba, SACCOS
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mkuu Wa Wilaya Komba Aitaka DIB Kuongeza Ulinzi Kwa Fedha Za Wananchi Katika Vikoba, SACCOS
Habari

Mkuu Wa Wilaya Komba Aitaka DIB Kuongeza Ulinzi Kwa Fedha Za Wananchi Katika Vikoba, SACCOS

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
GEITA: MKUU wa Wilaya ya Geita, Hashim Komba, ameitaka Bodi ya Bima ya Amana (DIB) kushuka hadi ngazi za chini zaidi, Ili kuhakikisha usalama wa mitaji ya wananchi wanaowekeza kwenye taasisi ndogondogo zisizo rasmi kama Vikundi vya Kuweka na Kukopa (VIKOBA) na Vyama vya Akiba na Mikopo (SACCOS).”
Komba ametoa rai hiyo alipotembelea banda la DIB kwenye maonesho ya nane ya Sekta ya Madini yanayoendelea mkoani Geita.
Habari Picha 9630
Amesema wananchi wengi wamekuwa wakipoteza fedha nyingi kutokana na kuwekeza kwenye vikundi visivyosajiliwa au visivyo chini ya usimamizi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
“Mara nyingi wananchi wanakuja ofisini kwetu wakilalamika kuwa wamepoteza fedha nyingi, wengine hadi Sh milioni 30, walizowekeza kwenye hisa au vikundi ambavyo si rasmi. Tunaanza kuhangaika kutafuta viongozi wa vikundi hivyo,” amesema.
Amesisitiza kwamba, ni muhimu kwa DIB kushirikiana kwa karibu na Benki Kuu, serikali za mitaa pamoja na taasisi nyingine za kifedha kuhakikisha mifumo ya kifedha ya kijamii kama VICOBA inapata kinga ya kifedha kama ilivyo kwa benki rasmi.
Habari Picha 9631
Naye Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano wa Umma na Mawasiliano wa DIB, Lwaga Mwambande, amesema bodi hiyo inatambua changamoto hizo na iko tayari kushirikiana na wadau wote kuhakikisha usalama wa fedha za wananchi.
“Tunaishukuru sana ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa ushauri huu. Tunaendelea kushirikiana na Benki Kuu pamoja na wadau wengine ili kuhakikisha taasisi zote za fedha, kubwa na ndogo, zinakuwa chini ya uangalizi na miongozo bora ya usimamizi,” amesema Mwambande.
Amesema kwa sasa, DIB inalinda amana za hadi Sh Milioni 7.5, na asilimia 99 ya wananchi wenye akaunti katika mabenki wanalindwa iwapo benki itafilisika.
“Lengo letu si tu kuwafidia wananchi pale panapotokea matatizo, bali ni kujenga imani ya wananchi katika mfumo rasmi wa kifedha ili waendelee kuutumia, na hivyo kusaidia kukuza uchumi wa taifa,” aliongeza.
Wito huo wa Mkuu wa Wilaya umetolewa wakati ambapo matumizi ya mifumo ya kifedha isiyo rasmi yanaongezeka, hali inayohitaji usimamizi madhubuti ili kulinda fedha za wananchi na kuimarisha uchumi wa taifa.

You Might Also Like

Mgahawa unaotembea fursa kwa vijana, kutoa huduma ya unywaji wa kahawa

TDB Yaheshimisha Tasnia Ya Maziwa

Tume Yapongeza OCPD kwa Mabadiliko ya Sheria

Sababu Nne Zilizofanikisha Mafanikio Katika Uandikishaji

Serikali Inatoa Kipaumbele Kufikisha Umeme Taasis Zinazotoa Huduma Kwa Jamii- Kapinga

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mjadala wa Kidiplomasia Ya Kisayansi Wafanyika Marekani
Next Article Epukeni Mikopo Inayowafilisi,Tumieni Taasisi Zinazotambulika Na BOT – Mkuu Wa Wilaya Komba
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?