MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mbunge Ulanga Aweka Mikakati Kuufungua Mkoa wa Morogoro Kimaendeleo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mbunge Ulanga Aweka Mikakati Kuufungua Mkoa wa Morogoro Kimaendeleo
Habari

Mbunge Ulanga Aweka Mikakati Kuufungua Mkoa wa Morogoro Kimaendeleo

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA:  MBUNGE wa Ulanga,  Salim Hasham, amesema kipaumbele chake cha kwanza ni kuhakikisha barabara ya Ifakara hadi Ulanga inajengwa kwa kiwango cha lami, kama ilivyoahidiwa na Rais Samia Suluhu Hassan kupitia Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2025–2030.
Amesema hayo katika Viwanja vya Bunge leo Novemba 12, 2025 alipozungumza na Waandishi wa Habari.
Amesema jukumu lake kama mbunge ni kusimamia na kuhakikisha ahadi hiyo inatekelezwa, kwani barabara hiyo ni kiunganishi muhimu kwa wananchi wa Ulanga na maeneo jirani.
“Serikali tayari imeanza kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Kilombero–Lupilo–Songea, na tunategemea barabara hiyo itasaidia kufungua mkoa wa Morogoro na kuunganisha mikoa ya kusini,” amesema.
Pia amesema mkoa wa Morogoro una mpango wa kujenga barabara nyingine kutoka Mlimba hadi Njombe, lengo likiwa ni kuhakikisha miundombinu ya usafiri inaimarika na kufungua fursa za kiuchumi katika maeneo yote ya mkoa huo.
Katika sekta ya Afya, amesema anapigania ujenzi wa hospitali mpya ya wilaya ndani ya Jimbo la Ulanga ili kuwapunguzia wananchi adha ya kusafiri umbali mrefu kutafuta huduma bora za afya.
“Hospitali ya sasa ni ya zamani na chakavu. Tunahitaji kituo kipya cha kisasa kitakachokidhi mahitaji ya wananchi wetu,” amesema..
Pia kwenye eneo la Kilimo na Umwagiliaji amesema,  jimbo la Ulanga limebahatika kuwa na miradi minne ya skimu za umwagiliaji ambayo tayari imefanyiwa upembuzi yakinifu. Miradi hiyo ipo katika kata za Mpande, Mbuga (Ruaha), Kichangani na Minepa.
Lengo ni kuongeza uzalishaji wa mazao na kuinua kipato cha wakulima wa Ulanga. Katika Sekta ya Madini amesema jimbo hilo lina mradi mkubwa wa uchimbaji na uchenjuaji wa madini ya graphite, uliyozinduliwa hivi karibuni na Waziri wa Madini.
Mradi huo wenye thamani ya Sh. Trilioni 1.3 unatarajiwa kutoa zaidi ya ajira 1,000 za kudumu na zaidi ya ajira 2,000 za muda, jambo litakaloinua uchumi wa eneo hilo.
“Huu ni mradi mkubwa utakaofungua uchumi wa Ulanga. Kupitia CSR, tunatarajia kuona maendeleo makubwa kwenye huduma za jamii, miundombinu na biashara,” amesema.
Akizungumzia Mapato na Maendeleo Endelevu, amesema  Kwa sasa, Jimbo hilo linakusanya kati ya Sh. Bilioni 2.5 hadi tatu kwa mwaka, lakini mbunge huyo anatarajia kiwango hicho kitaongezeka maradufu kutokana na uwekezaji mpya unaoendelea.
Amehimiza wananchi wa Ulanga kutambua na kutumia fursa zitakazotokana na miradi ya maendeleo, hasa sekta ya madini, ili kuinua maisha yao na kukuza uchumi wa eneo hilo.
“Tukitumia vizuri fursa hizi, Ulanga itakuwa kitovu cha maendeleo katika mkoa wa Morogoro,” amesema.

You Might Also Like

Madini Yaweka Rekodi Makusanyo Ya Maduhuli

Msisubiri Kupewa Amri, Ufanyaji Usafi Kwenye Maeneo Yenu – Lugendo

Bodi ya Bima ya Amana Yatoa  Bil 9.07 , Fidia Kwa Wateja Wa Benki Saba   Zilizofilisika

BRELA Yazindua Baraza La Wafanyakazi

MOI Yaokoa Bilioni 150 Matibabu Ya Kibingwa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Munde Aahidi Kuboresha Miundombinu, Uchumi Wa Liwale
Next Article Mwalunenge Kuunganisha Mbeya Mjini, Kusukuma Maendeleo Na Ajira Kwa Vijana
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Habari November 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?