MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: JAB yawaonya wanaofanya kazi za kihabari bila ithibati
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > JAB yawaonya wanaofanya kazi za kihabari bila ithibati
Habari

JAB yawaonya wanaofanya kazi za kihabari bila ithibati

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imebaini kuwa baadhi ya watu wasio na sifa za kitaaluma wameanza tena kutekeleza majukumu ya kihabari baada ya kukamilika kwa Uchaguzi Mkuu, Oktoba 29, 2025.
Akizungumza kuhusu hali hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Patrick Kipangula, amesema Bodi inawakumbusha wadau wote kuwa uandishi wa habari ni taaluma rasmi inayosimamiwa na misingi ya kisheria, maadili na weledi wa kitaaluma.
Amesisitiza kuwa mtu yeyote anayejihusisha na shughuli za kihabari bila kuwa na ithibati halali anakiuka masharti ya sheria.
Kipangula ameeleza kuwa makundi yanayotakiwa kuwa na ithibati ni pamoja na wahariri, waandishi wa habari, waandishi huru, wapiga picha za habari, wazalishaji wa vipindi pamoja na watangazaji wa redio na televisheni wanaofanya kazi katika vyombo vya habari.
“Kwa muktadha huo, Bodi inatoa onyo na kuwataka watu wote wanaotekeleza shughuli za kihabari bila kuwa na ithibati kuacha mara moja.
“Kuendelea kufanya hivyo ni kosa kisheria kwa mujibu wa Kifungu cha 50(2)(b) cha Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229,” amesema.
Ameongeza kuwa Bodi haitasita kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mtu au taasisi yoyote itakayobainika kuajiri au kuruhusu utekelezaji wa kazi za kihabari bila kufuata utaratibu na masharti yaliyowekwa kisheria.
Vilevile, JAB imeutaarifu umma na wadau wa sekta ya habari kuwa katika kipindi cha hivi karibuni itaendesha ukaguzi maalum katika vyombo vya habari na maeneo mbalimbali nchini.
Ukaguzi huo unalenga kujiridhisha kuwa wanaotekeleza majukumu ya kihabari wanakidhi vigezo vinavyotakiwa kwa mujibu wa sheria.
Bodi imetoa wito kwa wote wenye nia ya kufanya kazi za kihabari kuhakikisha wanapata ithibati halali, wanazingatia maadili na weledi wa juu wa taaluma, na kutumia kalamu, sauti na majukwaa yao kuwahudumia wananchi kwa kutoa taarifa sahihi, kukuza uwajibikaji na kuchangia maendeleo endelevu ya Taifa.

You Might Also Like

Ajali Yakatisha Maisha Ya Mkurugenzi  Mkuu Mtendaji TANESCO, Dereva Wake 

OCPD Yakabidhi Juzuu Mpya za Sheria kwa Ofisi ya Taifa ya Mashitaka

Wagonjwa 472 Waonwa Na Daktari Wa Mifupa MOI, 40 Wapendekezwa Kufika Dar kwa Matibabu

Serikali Yasisitiza Utoaji Huduma Bora Utekelezaji Bima Ya Afya

TUCTA: Wafanyakazi Jitokezeni  Kwa Wingi Kwenda Kupiga Kura Mchague Viongozi Watakaolinda  Maslahi Yenu  

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Vikao vya Kamati za Bunge Kuanza Januari 13, 2026 Dodoma
Next Article TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

CAG Aipongeza TARURA Kwa Ujenzi Wa Miundombinu
Habari January 9, 2026
Tuna Deni La Kusimamia Miradi Na Kusikiliza Kero za wananchi Ili Kuleta Maendeleo Ya Kweli-Salome
Habari January 9, 2026
Rais Dkt Samia Azindua Majengo Ya Kisasa
Habari January 8, 2026
TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar
Habari January 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?