MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: CCCC Yakutana na Wanahabari, Yapanga Mikakati Mipya 2025
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > CCCC Yakutana na Wanahabari, Yapanga Mikakati Mipya 2025
Habari

CCCC Yakutana na Wanahabari, Yapanga Mikakati Mipya 2025

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM:KAMPUNI ya Ujenzi na Mawasiliano ya China (CCCC), imesema mwaka mpya wa 2025 itajenga uhusiano bora na vyombo vya habari nchini Tanzania ili kuzitangaza kazi wanazozifanya kuhusu kampuni hiyo kwa viwango vipya.

Kiongozi wa tawi la CCCC nchini, Li Yuliang amesema hayo wakati wa hafla fupi ya wanahabari waliyoifanya ikiwa na lengo ya kutathmini mwaka unaoisha wa 2024, mipango ya 2025 pamoja na kuangalia maeneo yaliyokuwa na upungufu ili yaweze kuboreshwa.

Yuliang amesema, kukutana huko na wanahabari ni jambo zuri na mwanzo mpya wa ushirikiano wa kikazi baina ya pande zote mbili.

Amewashukuru wanahabari wote waliofanya nao kazi kwa mwaka uliopita wa 2024, kwa mchango wa kipekee wa kila chombo kuweza kufanikisha kuripoti taarifa zote za kampuni hiyo, ikiwa ni pamoja na kupokea ushauri wa nini kiboreshwe kwa mwaka unaokuja 2025.

Katika hafla hiyo kila chombo kiliweza kueleza shughuli inazozifanya, imeshiriki vipi katika kuandika habari za kampuni hiyo, na mikakati ya mwaka ujao.

Pia alielezea kuhusu taarifa ya maendeleo ya kampuni hiyo hapa nchini pamoja na miradi yake inayoifanya.

Naye Ofisa Msaidizi Ofisi ya Utawala katika kampuni hiyo ya CCCC, Yu Zixuan amesema pamoja na maendeleo waliyonayo katika soko la Tanzania, vyombo vya habari vimekuwa ni daraja katika maendeleo hayo kupitia usambazaji wa habari zake.

“Vyombo vya habari vina jukumu muhimu katika kuunda taswira ya shirika na kuongeza ufahamu wa umma,” amesema na kuongeza kuwa, hafla hivyo imelenga kujenga jukwaa la mazungumzo baina yake na vyombo vya habari ili kujadili mwelekeo wa maendeleo ya sekta yao.

“Kupitia tukio hili, tunatarajia kufanya kazi pamoja na marafiki zetu wa vyombo vya habari ili kuchangia katika kukuza maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya Tanzania.

“Kupitia majadiliano ya wazi wazi, tutaimarisha zaidi uhusiano kati ya tawi na vyombo vya habari, kukuza uboreshaji wa jumla wa shirika,” amesema.

Amesisitiza kuwa mwaka huu 2024 ni kumbukumbu ya miaka 75 tangu kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China na miaka 60 ya kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya China na Tanzania.

You Might Also Like

Ridhiwani Aiagiza CMA Kushughulikia Migogoro Kwa Haraka, Ufanisi

Walimu Kupatiwa Mafunzo ya Tehama

Mbegu Bora za Miwa Zenye Tija ya Tani 200 kwa Hekta Zaendelea Kuwanufaisha Wakulima

TEA, TotalEnergies Marketing Ltd Wakabidhi Madawati 130 Wilayani Kibiti

TDB Yaheshimisha Tasnia Ya Maziwa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Dkt. Biteko Afuta Likizo Za Watumishi Wote Tanesco
Next Article China Inaongoza Sekta ya Miundombinu na Ujenzi Tanzania
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mbegu Bora za Mpunga Zazalishwa TARI Dakawa, Ifakara
Habari August 7, 2025
Mtego wa Inzi Wa Matunda Suluhisho Salama kwa Wakulima
Habari August 7, 2025
Mafua, Kifua Yadaiwa Kusababisha Kifo cha Job Ndugai
Habari August 7, 2025
Zimbabwe Yakabidhi Uenyekiti Kwa Madagascar
Habari August 7, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?