Na Lucy Lyatuu,Dodoma
UTAFITI wa Uwezeshaji Wanawake Na Lishe 2023/24 umebaini kuwa wanawake asilimia 26 pekee nchini ndio wanaoamini wanaweza kuwa na uhuru wa kuwa na maamuzi ya kufanya shughuuli za kiuchumi.
Aidha asilimia 34.1 pekee ndio wanaunga mkono wanawake kuwa na uhuru wa kufanya maamuzi ya ndoa,talaka na uzazi nchini.
Waziri wa Maendeleo Ya Jamii, Jinsia Wanawake Na Makundi Maalum,Dkt Dorothy Gwajima amesema hayo wakati akizindua tafiti mbili zilizofanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) ambazo zinalenga kuweka bayana hali halisi ya takwimu na namna ya kutatua changamoto katika eneo husika.
Akizungumza,amezitaja tafiti zilizofanywa na NBS ni pamoja na unaouhusu mazingira na jinsia kwa mwaka 2025 pamoja namuwezeshaji wanawake na lishe 2023/24 ambazo,ni za kwanza kufanyika Tanzania na kwa bara la Afrika ni wa pili baada ya nchi ya Senegal.
Amesema kufanyika kwz tafiti hizo ni hatua kubwa ya maendeleo ya kiutafiti na inatoa changamoto kwa fursa zinazoikabili Tanzania,zinatoa ushahidi juu ya mazingira yaliyopo nchini zikiangazia nani aliyeathirika zaidi na kusaidia kupunguza pengo za kiashiria na kuongeza wigo wa uzalishaji tafiti.
Amesema asilimia 54.6 wanakataa aina zote za unyanyasaji wote na ukatili wa kijinsia huku wanawake wakiongoza kwa kuwa na ushawishi wa muda kwa asilimi 43.3 dhidi ya wanaume ambao ni asilimia 39.4.
Kuhusu fedha na matumizi,utafiti umebaini wanawake wako nyuma kwenye elimu ya matumizi ya fedha kwa asilimia 39.9 huku wanaume wakiwa na asilimia 54.8.Aidha wanawake wamekuwa wakishiriki katika vikundi visivyo rasmi na kwenye majukwaa ya dini.
“Kwa hali hiyo ipo hajamya elimu kwa wanawake kuhusu masuala ya fedha ikaongezwa ili kundi hilo liweze kukombolewa na kuongeza mchango wake wa maendeleo kwa taifa,”amesema na kuongeza kuwa utafiti wa mazingira umebaini wanawake kukumbwa na mabadiliko ya tabia nchi kwa asilimia 82.9.
Awali akizungumza Mwenyekiti wa bodi ya Takwimu, Anne Makinda amesema takwimu ndio dira ya Taifa na zimekuwa na msaada kuendeleza nchi.
Mtakwimu Mkuu wa,NBS, Dkt Amina Mrengwa amesema tafiti zilizozinduliwa ni adimu kufanywa nchini na zinasaidia kujibu viashiria mbalimbali vya maendeleo nchini.
Amesema matokeo ya tafiti hizo ni umuhimumwzke unaonekana katika utekelezaji wa dira ya Taifa ya Mwaka 2050 kuwa na uchumi imara na jumuishi na uwekezaji na kuongeza tija.

