MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: UDSM Imekuja Na App Inayounganisha Wakulima na Watoa Huduma za Kilimo kwa Haraka
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > UDSM Imekuja Na App Inayounganisha Wakulima na Watoa Huduma za Kilimo kwa Haraka
Habari

UDSM Imekuja Na App Inayounganisha Wakulima na Watoa Huduma za Kilimo kwa Haraka

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: CHUO Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), kimeanzisha teknolojia mpya kupitia programu ya simu janja inayolenga kuboresha upatikanaji wa huduma za kilimo kwa wakulima nchini.
Mhadhiri Msaidizi wa UDSM katika Idara ya Uhandisi wa Kilimo, Vicent Tsoray amesema hayo katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa na Kimataifa mkoani Dodoma.
Amesema Programu hiyo imeundwa kwa mfumo wa kipekee wenye sehemu mbili kuu moja kwa ajili ya wakulima na nyingine kwa watoa huduma wa kilimo.
Amesema Watumiaji wataweza kujisajili kama wakulima au watoa huduma kwa kuweka taarifa zao muhimu kama majina na nywila, ili kupata ufikiaji kamili wa huduma zilizopo kwenye programu hiyo.
“Kupitia APP hiyo, mkulima ataweza kuchagua huduma anayohitaji iwe ni upatikanaji wa mashine za kilimo kama matrekta, mashine za kuvunia, vifaa vya kunyunyizia dawa au kusambaza mbolea na kuainisha ukubwa wa shamba pamoja na aina ya mazao anayolima.
“Mfumo utamuonyesha orodha ya watoa huduma waliopo, na mkulima ataweza kuchagua mmoja kulingana na mahitaji yake,” amesema.
Amesema mtoa huduma atakapopokea ombi hilo, mfumo utaelekeza hatua kwa hatua jinsi huduma itakavyotolewa hadi kukamilika.
Teknolojia hii inalenga kuongeza ufanisi, kupunguza gharama na muda wa upatikanaji wa huduma za kilimo, na hivyo kuinua tija ya wakulima wadogo na wa kati.

You Might Also Like

Nguvu Zaidi Iongezwe Kwenye Tafiti Zinazogusa Maisha Ya Jamii

TUCTA Yakutana Na Mkuu Wa Mkoa Mbeya, Maandalizi Mei Mosi kitaifa 2025.

Watafiti Watumia Mbinu Mpya Kudhibiti Mdudu Kantangaze Kwenye Nyanya Bila Viuatilifu

OUT Yasaini Mkataba Ujenzi Wa Maabara Tatu Za Sayansi

Wakazi Wa Ntyuka Wataka Kiongozi Mchapakazi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Malecela Aibuka Kidume Dodoma Mjini, Mavunde Ang’aa Mtumba
Next Article UDSM Yaanzisha Mkakati Kuokoa Nyuki Wadogo
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mgodi Wa Dhahabu Wa Nyanzaga Kunufaisha Wananchi, Ujenzi Wazidi Kupaa
Habari September 23, 2025
Sekta Ya Madini Yazidi Kuchangia Ukuaji Wa Uchumi – Majaliwa
Habari September 23, 2025
Waziri Mkuu Majaliwa Akabidhi Tuzo kwa BoT Geita
Habari September 22, 2025
BoT Yarahisisha Uuzaji wa Dhahabu kwa Wachimbaji, Yatoa Punguzo La Mrabaha
Habari September 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?