MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kisaro Ahojiwa Kuhusu Migogoro ya Ardhi,  Mwinje Ajitosa na Suluhisho la Miundombinu na Umiliki wa Ardhi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kisaro Ahojiwa Kuhusu Migogoro ya Ardhi,  Mwinje Ajitosa na Suluhisho la Miundombinu na Umiliki wa Ardhi
Habari

Kisaro Ahojiwa Kuhusu Migogoro ya Ardhi,  Mwinje Ajitosa na Suluhisho la Miundombinu na Umiliki wa Ardhi

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Danson Kaijage
Migogoro ya ardhi imeendelea kuwa changamoto kubwa kwa wakazi wa Mkoa wa Dodoma, hasa katika Jimbo la Dodoma Mjini. Wananchi wamekuwa wakilalamikia vitendo vya uvamizi, ukosefu wa hati halali za umiliki, pamoja na madai ya mashamba kunyang’anywa bila fidia.
Suala hilo pia limekuwa kikwazo kwa mgombea ubunge wa Jimbo la Dodoma Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samwel Kisaro, ambaye amejikuta akilazimika kujibu maswali magumu kutoka kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho.
 Wajumbe hao wanadai Kisaro anamiliki kampuni inayojihusisha na upimaji, ununuzi na uuzaji wa ardhi, jambo linaloibua hofu ya mgongano wa maslahi endapo atachaguliwa kuwa mbunge.
“Ndugu mgombea, unatafuta ridhaa ya kuwa mbunge wa Dodoma Mjini, lakini tunakabiliwa na migogoro mingi ya ardhi. Inasemekana una kampuni ya upimaji, je, tukikuchagua utatusaidiaje kupata ardhi yetu bila kuingilia kwa maslahi binafsi?” alihoji mmoja wa wajumbe kutoka Kata ya Ntyuka.
Mjumbe mwingine, Anna Mputa, aliongeza kuwa kuna mashamba yaliyotwaliwa kinyume cha sheria na kutolewa kwa watu wenye uwezo kifedha, huku wamiliki halali wakiachwa bila fidia yoyote.
Akijibu tuhuma hizo, Kisaro amekanusha kumiliki kampuni ya upimaji wa ardhi, japokuwa alithibitisha kuwa anamiliki kampuni nyingine isiyohusiana na shughuli za upimaji.
Ameahidi kushughulikia tatizo hilo kwa kupendekeza mabadiliko ya sheria za ardhi ili kulinda haki za wananchi.
“Nikipewa ridhaa ya kuwa mbunge, nitahakikisha wale wote waliodhulumiwa ardhi yao wanapata haki zao kwa mujibu wa sheria. Tutapitia upya sheria za ardhi kuhakikisha kila mmoja ananufaika kwa haki,” amesema.
Katika hatua nyingine, mgombea mwenzake kupitia CCM, Robert Mwinje, ametumia jukwaa hilo kuwasilisha ajenda yake kwa wajumbe wa chama, akiahidi kushughulikia matatizo ya ardhi, miundombinu na mgawanyo wa ardhi kwa haki.
Akizungumza katika mkutano wa CCM Kata ya Ntyuka, Mwinje amesema amekuwa akihudumu ndani ya chama kwa muda mrefu kama Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Dodoma, hivyo anauelewa vizuri mkoa huo na changamoto zinazowakabili wananchi.
Licha ya kuachishwa nafasi hiyo kwa tuhuma ambazo hakuzifafanua, Mwinje ameeleza kuwa bado ana dhamira safi na uwezo wa kulitumikia jimbo hilo kwa ufanisi.
Ametaja vipaumbele vyake kuwa ni
 kutatua migogoro ya ardhi kwa kushirikiana na taasisi husika,
Kuboresha miundombinu ya barabara ili kuwezesha maendeleo ya kiuchumi.
Vile vile kuweka mfumo thabiti wa mgawanyo na umiliki wa ardhi ili kuondoa migogoro ya mara kwa mara.
Amekiri changamoto hizo zimekuwa kikwazo kikubwa kwa maendeleo ya wananchi na zinahitaji mbunge mwenye uelewa wa ndani ya jamii na dhamira ya kweli.

You Might Also Like

Kamati Ya Bunge Yaridhishwa Na Utaratibu Wa Manunuzi Ya Bando

NIT Yasema Ina Uwezo Wa Kufundisha Kozi Ya Urubani

TARI: Mabadiliko Ya Tabia Nchi Yamepunguza Ufanisi Wa Mbegu

Mbunifu Alilia Uwepo Wa Miongozo Kwa Wagunduzi

Mpogolo Aipongeza Halmashauri Maandalizi Mikopo Asilimia 10

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Rais Samia Aipa Neema Miradi Ya Kuzalisha Umeme Iringa
Next Article Wakazi Wa Ntyuka Wataka Kiongozi Mchapakazi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Jaji Mwambegele: Habari Sahihi ni Msingi wa Ushiriki Mpana wa Wananchi Kura 2025
Habari August 2, 2025
TARURA Yatoa Elimu Nane Nane
Habari August 2, 2025
Wakazi Wa Ntyuka Wataka Kiongozi Mchapakazi
Habari August 1, 2025
Rais Samia Aipa Neema Miradi Ya Kuzalisha Umeme Iringa
Habari August 1, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?