MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Rais Mpya CWT Ikomba: ‘Nataka Kuwaunganisha Walimu, Kuitendea Haki Kazi Yetu’
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Rais Mpya CWT Ikomba: ‘Nataka Kuwaunganisha Walimu, Kuitendea Haki Kazi Yetu’
Habari

Rais Mpya CWT Ikomba: ‘Nataka Kuwaunganisha Walimu, Kuitendea Haki Kazi Yetu’

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
9Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: RAIS wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Mwalimu Suleiman Ikomba ameelezea dhamira yake ya kuwaleta walimu pamoja, kuwatumikia kwa uadilifu, na kuijenga upya taswira ya taaluma ya ualimu kama uti wa mgongo wa taifa.
Ikomba ameelezea hayo alipozungumza na Mfanyakazi Tanzania kuhusu dhamira yake kwa CWT baada ya kuchaguliwa kuwaongoza walimu kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia 2025 hadi 2030.
Amesema uamuzi wake wa kugombea nafasi ya urais ulitokana na wito wa dhati wa kuwatumikia walimu, licha ya changamoto na mitazamo tofauti iliyokuwepo.
“Miaka mitano ilipofika, tulihitaji viongozi wapya. Nilitafakari sana kabla ya kugombea. Nilijua kabisa kwamba nafasi hizi si za kujitwalia kibinafsi bali ni dhamana ya wanachama.
“Nilikuwa tayari kama nitashinda au kushindwa, kurudi kwenye kazi yangu, lakini dhamira yangu ilikuwa kuhakikisha chama kinakuwa cha wanachama na si cha watu wachache,” amesema.
Ameeleza kwamba kazi kubwa iliyo mbele yake sasa ni kuunganisha walimu wote nchini bila kujali tofauti za kiitikadi, kijiografia au vyeo.
Amesisitiza kuwa maendeleo ya kweli ya walimu hayawezi kufikiwa bila mshikamano wa kweli na mawasiliano ya wazi kati ya uongozi na wanachama.
 “Lazima tuwasaidie walimu kwa pamoja. Tuone matatizo yao na tuwaoneshe njia ya kuyatatua. Sisi kama watumishi wa umma, lazima tufikiri njia bora zinazotufaa wote, si kwa masilahi ya wachache,” amesema.
Ikomba amegusia pia kuibuka kwa vyama vingine vya walimu nchini, akisema ni muhimu kuchunguza kiini chake, kusikiliza sababu za kuibuka kwake, na kujifunza.
Amesisitiza kuwa chama cha walimu kinapaswa kusimama kama sauti ya kweli ya walimu wote, na kuhakikisha kila mwalimu anahisi kusikilizwa na kuheshimiwa.
“Lazima tuelewe vyanzo vya migawanyiko. Tujue walimu wana shida zipi hadi wanatafuta sehemu nyingine ya kujiunga. Chama hiki ni cha wanachama tunawajibika kujifunza, kusahihisha, na kuboresha,” amesema.
Pia ametoa ahadi kwa walimu  kuwatumikia kwa ukamilifu na kuhakikisha kuwa changamoto zinazowakumba zinapatiwa majibu.
“Nataka kuona walimu wanapata matunda bora ya kazi yao. Nataka kuwaona wakifurahia kazi yao kwa sababu mazingira yao yameratibiwa vizuri. Naomba tushirikiane ili kazi yetu ya ualimu ibaki na hadhi na ubora unaostahili,” amesema.

You Might Also Like

Atoa Maelekezo Kwa Chuo Cha Hombolo Kuwajengea Uwezo Viongozi Wa Mitaa Na Vijiji -Kapinga

Majaliwa Asema Sekta ya Uvuvi Yaingiza trilioni 2.9 kwa Mwaka 

Kasulu Yatoa Mafunzo Utumiaji wa Mfumo Wa Kieletroniki Kwa Wakuu wa Divisheni, Vitengo

CHAUMMA Yataka Kuvunja Bodi ya Korosho, Kuunda Mamlaka Mpya ya Mazao ya Kimkakati

Februari Mwaka Huu Wafanyabiashara Kariakoo Kurejea, Wenye Madeni Waagizwa Kulipa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Tumeleta Utulivu na Huduma kwa Walimu’ – Ikomba
Next Article Rais CWT Asikitishwa Na Uzembe, Maofisa Wa Halmashauri
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Twendeni Tukapige Kura Ya Ukombozi, CHAUMMA Yahitimisha Kampeni
Habari October 28, 2025
Elimu Ya Nishati Safi Ya Kupikia Yawafikia Maofisa Dawati Ngazi Ya Mikoa Na Halmashauri
Habari October 27, 2025
Wananchi wahamasishwa kuandika historia mpya kupitia kura
Habari October 25, 2025
Shibuda: WanaMaswa jitokezeni kupiga kura bila woga
Habari October 25, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?