MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: NBS: Utumiaji Wa Takwimu Nyenzo Muhimu Kwa Mama Lishe
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > NBS: Utumiaji Wa Takwimu Nyenzo Muhimu Kwa Mama Lishe
Habari

NBS: Utumiaji Wa Takwimu Nyenzo Muhimu Kwa Mama Lishe

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: MTAKWIMU Mwandamizi kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Boniface Simpoli, amesema takwimu si kwa ajili ya wataalamu peke yao, bali ni nyenzo muhimu kwa kila mwananchi, wakiwemo wafanyabiashara wadogo.
Amesema hayo alipozungumza na Mwandishi wa habari hii katika maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara yajulikanayo kama Sabasaba yanayoendelea mkoani Dar es Salaam.
 “Takwimu ni mwanga. Ukishakuwa na huo mwanga, hata mama ntilie anaweza kupanga vizuri biashara yake na kuikuza,” anasema Simpoli.
Kwa mujibu wa Simpoli, NBS huzalisha takwimu rasmi katika makundi matatu makuu ya kijamii, kiuchumi na mazingira.
Amesema takwimu hizo zina taarifa muhimu zinazoweza kumsaidia mama ntilie kupanga kwa ufanisi, kufuatilia mwenendo wa soko, na kujua wapi kuna fursa zaidi za biashara.
Takwimu za kijamii, kama zile zilizotokana na Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, zinaweza kutoa mwanga kwa mama ntilie kuhusu wapi afanye huduma zake.
 “Kwa mfano, akijua kuwa mtaa fulani una idadi kubwa ya wanaume ambao hawajaoa, anaweza kufungua mgahawa wake hapo kwa sababu kuna uwezekano mkubwa kuwa hawapiki nyumbani. Hiyo ni fursa ya soko,” amesema.
Amesema takwimu hizo pia zinaonyesha idadi ya watu kwa jinsi, hali ya ndoa, na makadirio ya ongezeko la watu hadi mwaka 2050, taarifa ambazo ni muhimu kwa mfanyabiashara kupanga maendeleo ya muda mrefu.
Amesema mbali na takwimu za kijamii, mama ntilie anaweza kufaidika na takwimu za kiuchumi, hasa katika kilimo. Kwa mfano, kwa kujua mikoa yenye uzalishaji mkubwa wa mazao kama viazi, nyanya au maharage, anaweza kupanga manunuzi ya chakula kwa bei nafuu moja kwa moja kutoka mashambani, hivyo kupunguza gharama za uendeshaji.
“Ukijua wapi kuna uzalishaji mkubwa, na wapi kuna masoko yenye watu wengi, unaweza kupanga safari zako za manunuzi na usambazaji kwa faida zaidi,” amesema.
Kwa mfano, takwimu zinaweza kuonyesha kuwa Mkoa wa Iringa una uzalishaji mkubwa wa nyanya, huku Dar es Salaam ikiwa na soko kubwa la bidhaa hiyo. Mama ntilie anaweza kutumia taarifa hiyo kupanga biashara ya nyanya kwa ufanisi mkubwa.
Amesena Ofisi ya Taifa ya Takwimu inaendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa kutumia takwimu katika maisha ya kila siku.
 “Mama ntilie asione kama takwimu ni za maofisini tu. Ziko kwa ajili yake pia. Akizielewa, anaweza kufanya maamuzi bora zaidi, kupunguza hasara, na kuongeza kipato,” amesema.

You Might Also Like

Wazazi washauriwa kusomesha watoto useremala

Elimu Ya Fedha Yafika Makanya Same

Kafulila: Ushirikiano wa Sekta Binafsi na Umma Kuboresha Huduma

Kikosi Kazi Maalumu Cha Kupitia Muongozo Wa Ufasili Wa Sheria Chazinduliwa

Biteko Amwakilisha Rais Samia Harambee Ujenzi Kanisa Katoliki

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article FCC Yatoa Elimu Ya Ushindani Wa Kibiashara Katika Maonesho Ya  Biashara
Next Article THBUB Mdau Mkubwa Utekelezaji Wa Majukumu 
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Majaliwa Apongeza Jeshi La Magereza Kurasimisha Ujuzi Kwa Wafungwa
Habari August 27, 2025
Mapokezi Ya Katibu Mkuu CCM  Dkt Migiro CCM, Aahidi Ushirikiano
Habari August 27, 2025
Majaliwa Aagiza Kuimarishwa kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini
Habari August 27, 2025
VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani
Habari August 26, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?