MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Chalamila Akagua Miradi Jimbo La Kibamba Ubungo DSM
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Chalamila Akagua Miradi Jimbo La Kibamba Ubungo DSM
Habari

Chalamila Akagua Miradi Jimbo La Kibamba Ubungo DSM

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila ameagiza miradi kujengwa kwa viwango kulingana na thamani ya fedha, pia ikamilike kwa wakati uliowekwa.
Chalamila ametoa maagizo hayo alipofanya ziara ya kutembelea ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo Jimbo la Kibamba, Wilaya ya Ubungo Dar es Salaam.
“Ni muhimu kufanya ujenzi wa miradi unaozingatia thamani ya fedha, miradi inayoweza kudumu kwa miaka mingi na ujenzi ukamilike kwa wakati ili kumaliza adha kwa akina mama na watoto ” amesema.
Pia amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa pesa nyingi zinazowezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo alupokuwa akiweka Jiwe la Msingi katika mradi wa jengo la mama na mtoto kwenye kituo cha afya cha Mpiji Magoe
Pia akiwa kwenye mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari Goba Kulangwa Chalamila amesisitiza suala la ulinzi na usalama wakati nchi ikiwa inaelekea kwenye uchaguzi mkuu hivyo ameagiza kukamilishwa kwa ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Tegeta A.
Naye Meya wa Manispaa ya Ubungo Juma Nyaigesha amewataka wananchi na wafanyabiashara kuto kukwepa kulipa kodi kwani ndio chanzo cha kupata fedha za ujenzi wa miradi ya maendeleo ikiwemo vituo vya afya.
 Pia Mganga Mfawidhi wa kituo cha Afya Mpiji Magoe Hereswida Cosmas akieleza maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo la mama na mtoto amesema ujenzi unaendelea vizuri na utakamilika kwa wakati.
Vile vile Chalamila ametembelea na kukagua mradi wa maji wa kibamba, pamoja na kukagua mradi wa shule ya sekondari Goba Kulangwa.
Katika ziara hiyo amemalizia kwa kufanya mkutano wa hadhara Kata ya Saranga eneo la ofisi ya Serikali ya Mtaa na kusikiliza kero mbalimbali za wananchi ikiwemo ubovu wa barabara, changamoto ya TASAF, Maji, kusuasua kukamilika kwa ujenzi wa Zahanati ambapo ameahidi kabla ya kufika ijumaa ya wiki ijayo fedha zitakuwa zimepelekwa.
 .

You Might Also Like

TRA: Serikali imemgusa mkulima kupitia mabadiliko ya sheria

Tutuba: Noti Mpya Kuanza Kutumika Februari Mosi mwaka huu

Siri ya ushindi JKT hii hapa

Rais Samia Aridhia Malipo Ya Fidia Barabara Ya Afrika Mashariki

PSSSF sasa kidijitali

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TUCTA Yafuatilia Hotuba Ya Waziri Mkuu Bungeni
Next Article Matukio Mbalimbali Katika Picha Baada Ya Waziri Mkuu Kuwasilisha Makadirio Ya Mapato Ya Bajeti
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?