MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Silaa: Akili Mnemba, Roboti kuongeza ufanisi,ubunifu 
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Silaa: Akili Mnemba, Roboti kuongeza ufanisi,ubunifu 
Habari

Silaa: Akili Mnemba, Roboti kuongeza ufanisi,ubunifu 

Author
By Author
Share
3 Min Read
  1. Na Lucy Ngowi

TEKNOLOJIA za Akili Mnemba na Roboti zitasaidia kutatua changamoto mbalimbali nchini, kutokana na kuongeza ufanisi, kupunguza gharama, na kutoa ubunifu katika sekta mbalimbali.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry Silaa amesema hayo wakati wa ufunguzi wa Kongamano la nane la Mwaka la TEHAMA Tanzania.

Silaa ametolea mfano changamoto hizo zinazoweza kutatuliwa na teknolojia hiyo ya akili mnemba na roboti kuwa ni afya, kilimo, elimu, na usimamizi wa rasilimali.

Amesema kama ilivyo kwa nchi nyingi zinazoendelea,

Tanzania inakabiliwa na changamoto kwenye jamii zinazohitaji suluhisho la haraka na endelevu.

Pia amesema katika wizara anayoiongoza, mbali na majukumu mengine anasimamia Sera ya Tehama 2016 ambayo imebainisha masuala ya Kisera, Kisheria na Taasisi katika kukuza matumizi ya Tehama Nchini.

Amesema kongamano hilo alilolifungua lina kauli mbiu isemayo, ‘Kutumia Uwezo wa Akili Mnemba na Robotiki kwa Mapinduzi ya Kiuchumi na Kijamii’, kwamba inafungua mjadala muhimu kwa wakati huu ambao dunia nzima inashuhudia mapinduzi ya kidijitali.

Awali amesema serikali imeendelea kuwekeza kwa kasi kubwa katika Tehama ambayo ndio nguzo kuu ya kufikia Uchumi wa Kidijitali.

“Dunia hivi sasa ipo katika kipindi cha Mapinduzi ya Nne, Tano na Sita ya viwanda ambapo shughuli za kiuchumi, kijamii na uzalishaji kwa kiasi kikubwa inakwenda kuendeshwa kwa kutumia teknolojia za juu za Tehama,” amesema.

Amesema kwa umuhimu huo Serikali imeendelea kuwekeza katika kufanya maboresho ya Kisera, Kisheria na Kitaasisi pamoja na kujenga uwezo kwa Watanzania ili kuhakikisha kuwa Tanzania inakuwa sehemu ya mabadiliko katika masuala ya Tehama duniani.

Silaa amesema katika sekta ya afya, Akili Mnemba na Roboti inaweza kusaidia kutoa utambuzi wa haraka wa magonjwa na kuboresha huduma za afya za msingi.

“Katika kilimo, Akili Mnemba na Roboti inaweza kuboresha tija kwa wakulima kwa kusaidia katika usimamizi bora wa uzalishaji na utafiti wa hali ya hewa.

“Pia, teknolojia hii inaweza kubadilisha kabisa jinsi tunavyoendesha biashara na utengenezaji wa bidhaa, kwa kuboresha mifumo ya usambazaji na kuongeza ufanisi,” amesema.

Amesema kwa kutumia Akili Mnemba na Roboti, viwanda nchini vinaweza kuongeza uzalishaji na kuwa na ushindani mkubwa kwenye soko la kimataifa.

“Akili Mnemba na Roboti inaweza kuimarisha mifumo ya elimu kwa kusaidia upatikanaji wa elimu bora kwa kila mwanafunzi, bila kujali eneo au hali yake ya kiuchumi.

“Kwa njia hii, tunaweza kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anapata fursa ya kujifunza na kuchangia katika maendeleo ya taifa letu,” amesema.

You Might Also Like

Rais Samia Aongoza Waombolezaji Kutoa Heshima Za Mwisho Kwa Mbunge Ndungulile

Wakandarasi Miradi wa  TAZA Watakiwa Kukamilisha Kazi kwa Wakati 

BRELA kuanza kuwasajili wakulima

Spika Ahoji Mwongozo Wa Wanaojitolea Kazin

TARI Yakutanisha Wadau Kuwaeleza Matokeo Ya Tafiti Za Mbegu Wanazofanya

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Ridhiwani  Azindua Hafla ya Kuupandisha Mwenge, Mlima Kilimanjaro
Next Article Vijana Wahimizwa Kushiriki Kikamilifu Soko Huru la Afrika
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Tanzania, Belarus Zaanza Ukurasa Mpya wa Ushirikiano wa Kimkakati
Habari July 23, 2025
Rais Samia Atoa Bil. Nne Ujenzi Kiwanda Cha Kuzalisha  Nishati Mbadala  
Habari July 22, 2025
Ziara ya Kwanza ya Kiongozi wa Juu wa Tanzania Nchini Belarus Yafungua Ukurasa Mpya wa Ushirikiano
Habari July 22, 2025
Mapinduzi ya Elimu Geita: Wasichana Wamerudi Shule kwa Kasi
Habari July 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?