MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kongamano la Kahawa Bora Afrika kufanyika Tanzania Februari mwakani
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kongamano la Kahawa Bora Afrika kufanyika Tanzania Februari mwakani
Habari

Kongamano la Kahawa Bora Afrika kufanyika Tanzania Februari mwakani

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

WAZALISHAJI, wafanyabiashara na wakaangaji wa kahawa duniani wamealikwa kushiriki Kongamano na Maonyesho ya 21 ya Kahawa bora Afrika, yatakayofanyika Dar es Salaam, Februari 26 hadi 28 mwaka ujao 2025.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Kahawa Tanzania (TCB), Primus Kimaryo amesema hayo katika mkutano wa maandalizi ya kongamano hilo ulioandaliwa na bodi hiyo kwa kushirikiana na Chama cha Kahawa Bora za Afrika (AFCA).
Kimaryo amesema kongamano hilo linatoa fursa ya pekee kwa nchi ya Tanzania baada ya kufunguka kibiashara.
“Tanzania sasa uzalishaji wetu wa kahawa unaendelea kuongezeka,imekuwa ni fursa kwetu kuona ni namna gani tunaileta tena dunia ya kahawa hapa nchini.
“Kwa hiyo hii ni fursa pekee kwa wakulima wa kahawa na wadau wote wa sekta ya kahawa Tanzania kuionyesha ni namna gani tunavyoweza kupata masoko mapya, kutafuta masoko na kuonyesha kahawa zetu zote mbili ambazo ni Robusta na Arabica,” amesema.
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya AFCA, Amir Hamza amesema kilichoipa nguvu ya kuleta maonesho hayo Tanzania, ni kutokana na Rais Samia Suluhu Hassan kuifungua nchi kibiashara.
“Huu ni wakati sahihi wa wakulima kuonyesha ni nini inafanya katika kahawa kwa dunia,” amesema.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Masoko TCB, Frank Nyarusi amesema zaidi ya wakulima wadogo 320,000 wanategemea kahawa hapa nchini, pia watu milioni mbili wanaitegemea kahawa katika maeneo mbalimbali.
“Kahawa inaingiza dola za marekani mil 200 ni chanzo kikubwa cha mapato katika nchi,” amesema.
Amesema jitihada wanayoifanya ni kushirikisha wadau katika mnyororo wa kahawa, pia kutengeneza mazingira wezeshi ili kila mtu awekeze, auze na kufurahia fursa zote zilizopo kwenye kahawa.

You Might Also Like

Ajira kwa Vijana na Afya kwa Wazee: Ajenda Kuu za Wagombea Jimbo la Dodoma Mjini

Serikali Yaongeza Bajeti Mfuko Wa Utamaduni Na Sanaa

Wanaosimamia Mitandao Ya Serikali Wadhibiti Usalama Wake

TPHPA Tumejiimarisha Kudhibiti Visumbufu Vya Mazao – Ndunguru

Rais Samia Awatega Wateule Wake

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Biashara kidijitali inawezekana soko huru la Afrika
Next Article DAWASA na TARURA Kuendeleza Ushirikiano Ulinzi wa Miundombinu
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Serikali Yatoa Mwelekeo Maandalizi AFCON 2027, Yaimarisha Miundombinu Nchini
Habari April 17, 2026
Makampuni 100 kushiriki maonesho ya OSHA Njombe
Habari April 17, 2026
Ufaulu  Wa   Somo La Hisabati  Shida Ya Taifa- Wanu
Habari April 16, 2026
Ofisi ya Rais Mipango Yaomba Bilioni 144.85 kwa Bajeti 2026/27
Habari April 16, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?