MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Tanzania Mwenyeji Mkutano wa Mafuta na Gesi, 2025
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Tanzania Mwenyeji Mkutano wa Mafuta na Gesi, 2025
Habari

Tanzania Mwenyeji Mkutano wa Mafuta na Gesi, 2025

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Na Mwandishi Wetu

NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko ameshiriki katika kikao cha maandalizi ya Mkutano na Maonesho ya 11 ya Petroli ya Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAPCE’25).

Mkutano huo unatarajiwa kufanyika kuanzia Machi 5 hadi 7, 2025 katika ukumbi wa JNICC , Dar es Salaam.

Mkutano huo wa siku tatu utatanguliwa na safari za kutembelea maeneo ya kijiolojia na kujionea vivutio mbalimbali vya kitalii vilivyopo katika nchi wanachama wa jumuiya hiyo.

Aidha, watazungumzia masuala ya mabadiliko kuelekea katika matumizi ya nishati safi na kuwakutanisha wadau zaidi ya 1000 kutoka mataifa mbalimbali wanatarajiwa kushiriki katika mkutano huo.

Akizungumza katika kikao hicho, Dkt. Biteko amesema “Kama nchi tumepata fursa ya kuandaa mkutano huu wa kimataifa na Serikali imepanga kufanya hivyo kwa kushirikiana na sekta binafsi ili kuandaa mkutano wenye tija kwa nchi na kutoa nafasi kwa Watanzania kufaidika na uwepo wa mkutano huu”.

Dkt. Biteko ametoa rai kwa wahudhuriaji wa kikao hicho kutumia vema fursa ya uwepo wa mkutano wa EAPCE’25 kutangaza biashara, huduma na utaalamu wao pamoja na kujenga mitandao na washirika kutoka mataifa mbalimbali.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Felchesmi Mramba ameeleza kuwa mkutano wa EAPCE’25 pia utahusisha maonesho ya huduma na bidhaa mbalimbali na hivyo kutoa fursa kwa wadau kuchangamkia fursa hiyo.

“Sambamba na mkutano na maonesho eneo lingine ambalo wadau wanakaribishwa kuchangamkia ni udhamini wa mkutano ambao unatoa nafasi ya kujitangaza ndani na nje ya nchi kwa kuzingatia ukubwa wa mkutano wenyewe” amesema Mramba.

You Might Also Like

Tunaunga mkono jitihada za Rais Samia katika Utalii

Mafanikio Ya TEA Kwa Serikali Awamu Ya Sita;Miradi Ya Elimu 3,768 Yatekelezwa, Bil. 49.5 Zatumika

Profesa Mkenda Aitaka TAEC Kusomesha Watumishi

Kamati Ya Bunge Yahimiza Maslahi Ya Watumishi Wapya Yazingatiwe

OUT Yawanoa Watumishi Wa Mamlaka Za Serikali Za Mitaa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Shilingi bilioni 4.6 kupeleka umeme maeneo ya migodi
Next Article Tumeridhika na kazi za TTCL – Mwanaisha
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

CAG Aipongeza TARURA Kwa Ujenzi Wa Miundombinu
Habari January 9, 2026
Tuna Deni La Kusimamia Miradi Na Kusikiliza Kero za wananchi Ili Kuleta Maendeleo Ya Kweli-Salome
Habari January 9, 2026
Rais Dkt Samia Azindua Majengo Ya Kisasa
Habari January 8, 2026
TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar
Habari January 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?