MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Sheria ya ajira, mahusiano kazini ipitiwe upya
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Sheria ya ajira, mahusiano kazini ipitiwe upya
Habari

Sheria ya ajira, mahusiano kazini ipitiwe upya

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
SHERIA ya Ajira na Mahusiano Kazini imekuwa ikichanganya watumishi,hali inayosababisha ucheleweshaji wa kumaliza migogoro ya wafanyakazi.
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Reli Tanzania (TRAWU), Edo Makata amesema hayo alipozungumza na Gazeti la Mfanyakazi.
Amesema kutoka na mkanganyiko huo, wafanyakazi wenye migogoro na mwajiri wanaweza kukaa miaka mitatu mpaka minne hawajapata majibu yao.
“Ama unakuta mfanyakazi anaweza kurudishwa kazini lakini mwajiri wake anakuwa hamhitaji,” amesema.
Amesema changamoto hiyo imejitokeza kwa wafanyakazi waliondolewa ambao hawakuwa na vyeti vya elimu ya kidato cha nne.
Kwamba waliokuwa Wafanyakazi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), wamekumbwa na changamoto kutokana na shirika hilo huko nyuma kuajiri wasiokuwa na sifa ya cheti cha kidato cha nne.
“Ilipofika muda wa kutekeleza matakwa ya serikali kwa nyaraka mbalimbali zilizotumwa TRC,wafanyakazi wengi waliondolewa wasiokuwa na elimu ya kidato cha nne, pia wasiokuwa na vyeti.
“Hii ilikuwa ni shida sababu wameshaajiriwa, wamekaa humo, ila matakwa ya serikali kwa mujibu wa nyaraka, walihitajika watoe vyeti vyao. Hili limekuwa ni tatizo kubwa kwa sababu walioondolewa kwenye mshahara hawakujua hatma yao.
“Hizi kesi zimekuwa ni nyingi zimeendelea kupelekwa kwenye Tume ya Utumishi wa Umma kama chombo ambacho kinasikiliza rufaa ambazo zinaendelea kwa watumishi wa umma kwa sababu sekta zote mbili zimeonekana sekta za umma kwa asilimia 100,” amesema.
Pia ameeleza changamoto nyingine kwa watumishi wanaofukuzwa kazi kwa sababu mbalimbali, endapo kesi itapelekwa Tume ya Utumishi wa Umma, na ikatokea mfanyakazi ameshinda, mwajiri hukata rufaa kwa Rais.
Amesema mwajiri anapokata rufaa huchukua muda mrefu kuiamua huku mfanyakazi anasota bila ajira japo tume imeamua arejeshwe kazini.
Akizungumzia upande wa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara), wafanyakazi wengi walipeleka kesi zao Tume ya Usuluhishi na Upatanishi, lakini kupitia mahakama kesi hizo zilionekana zimepelekwa Tume ya Utumishi wa Umma.
“Sasa tume inakaa muda mrefu kuweza kufanya maamuzi yake kwa muundo wake,” amesema.

You Might Also Like

Ofisi Ya Taifa Ya Takwimu  Kufanya Tafiti Kwa Wakala Wa Huduma Za Fedha,Viwandani

Rais Wa CWT Suleiman Ikomba Sasa Ni Daktari

Kipaji pekee hakitoshi katika kufanya kazi za kihabari – Kipangula

MAIPAC Yagawa Bure  Majiko Ya Gesi Monduli, Lowassa Apongeza.             

Ridhiwani Kikwete Ajiandikisha Kupiga Kura Kijijini Msoga

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TRAWU yapigania mkataba hali bora za kazi miaka 11 sasa
Next Article Dada wa kazi aliyejeruhi akamatwa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Wizara Ya Nishati Kutekeleza Dira Ya Taifa 2050,Kuhamasisha Matumizi Ya  Nishati Safi
Habari April 21, 2026
Mandingo: Jiungeni Mkunga Marathon Kuokoa Maisha ya Mama na Mtoto
Habari April 21, 2026
‘Upungufu wa Wakunga Afrika Watishia Maisha ya Mama na Mtoto ‘TAMA
Habari April 21, 2026
Serikali Yatoa Mwelekeo Maandalizi AFCON 2027, Yaimarisha Miundombinu Nchini
Habari April 17, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?