Na Lucy Lyatuu,Morogoro
KUELEKEA mashindano ya mpira wa miguu kwa bara la Africa Afcon, Mamlaka Ya Elimu Na Mafunzo Ya Ufundi Stadi (VETA) imesema imejiandaa vyema na kuwataka vijana na wanafunzi wao kutumia fursa hiyo ya mashindano kuonesha bidhaa zao pamoja na kutoa huduma bora.Mratibu wa Uandaaji Wa Mitalaa kutoka VETA Happynes Salema amesema hayo wakati akizungumza katika banda la VETA katika tamasha la Kitaifa la nne La Utamaduni linaloendelea mkoani Morogoro.Akizungumza Salema amesema Mamlaka hiyo VETA ina vyuo 15 vinavyotoa mafunzo ya sekta ya utalii na ukarimu na katika mafunzo hayo yanaenda pamoja na dhana ya utamaduni.

Amevitaja vyuo vinavyotoa mafunzo ya hoteli kuwa vipo eneo la Njiro,Moshi, Tanga, Mbeya ,Mtwara na kuwataka wanafunzi popote wajijnge na Mamlaka hiyo kupata huduma.Amesema katika kipindi hicho cha mashindano, VETA imejiandaa kutoa huduma kwa kipindi chote na kwa kutumia hoteli zao wamejiandaa kutoa huduma.“Kwa mfano pale Njiro mkoani Arusha kuna hoteli yetu ya nyota tatu ambapo vijana na wanafunzi waliosoma fani mbalimbali za upishi na sanaa wanaandaliwa kubuni vitu mbalimbali ikiwemo shanga za kimasai,nguo za kiutamaduni na vikoi kwa ajili ya kuhufumia watanzania na wageni.Kuhusu utalii amesema VETA kupitia vyuo vyake wanafunzi wanafundishwa namna ya kulinda utamaduni na kujifunza kucheza ngoma za asili kulingana na makabila tofautitofautu yaliyopo nchini Tanzania.Amesema katika tamasha la utamaduni wmeleta wanafunzi kuonesha umahiri wa kucheza ngoma kwa ajili ya fani ya utalii pia kuleta ubunifu wa mavazi ambayo yanaakisi utamaduni wa watanzania.

