MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Qwaray Aipongeza VETA kwa Kukuza Ujuzi wa Vijana
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Qwaray Aipongeza VETA kwa Kukuza Ujuzi wa Vijana
Habari

Qwaray Aipongeza VETA kwa Kukuza Ujuzi wa Vijana

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: NAIBU Waziri wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Regina Qwaray, ameipongeza Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) kwa mchango wake katika kuwajengea vijana ujuzi unaowawezesha kujiajiri na kuchangia maendeleo ya uchumi wa nchi.
Akizungumza baada ya kutembelea banda la VETA katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma Juni 22, 2026, Qwaray amesema Serikali imejikita katika kuwawezesha vijana kujiajiri, jambo ambalo litafanikiwa zaidi kupitia uwekezaji mkubwa katika elimu ya ufundi na stadi za kazi.
“Vijana wanapopata ujuzi wa ufundi wanakuwa na uwezo wa kujitegemea kiuchumi badala ya kusubiri ajira za Serikali. Hivyo, ni muhimu kuendelea kuwekeza katika vyuo vya VETA ili kuongeza fursa za ajira na uzalishaji,” amesema.
Habari Picha 12575
Qwaray pia ameipongeza VETA kwa kutoa mafunzo kwa watu wenye mahitaji maalum na kwa juhudi zake za kuzalisha bidhaa mbalimbali kupitia kampuni tanzu ya VETA Ujuzi, hatua inayochangia kukuza uchumi na kuongeza thamani ya mafunzo yanayotolewa.
Amesema wahitimu wa elimu mbalimbali, ikiwemo kidato cha nne na elimu ya juu, wanapaswa kutumia fursa zinazotolewa na VETA kupata stadi zinazowawezesha kujiajiri na kuanzisha shughuli za uzalishaji.
Aidha, amebainisha kuwa maendeleo ya ujuzi kwa wananchi ni nguzo muhimu katika kufanikisha malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, inayolenga kujenga uchumi wa kisasa unaotegemea maarifa na ubunifu.
Habari Picha 12578
VETA ni miongoni mwa taasisi zinazoshiriki katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyoanza Juni 16, 2026, kufunguliwa rasmi Juni 17 na Waziri wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, na yanatarajiwa kuhitimishwa Juni 23, 2026.

You Might Also Like

Watanzania Tuendelee Kudumisha Amani-Dk Biteko

Mwalim: Nikichaguliwa urais, Kigaila atakuwa Waziri Mkuu wangu

Takukuru Kinondoni Yapokea Malalamiko 46 Kuhusu Rushwa

DIT Andaeni Taarifa  Itakayowezesha Wanafunzi Kupelekwa Nje Kujifunza-Mkenda

Vyuo vya Kilimo vishirikishwe mradi wa BBT

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mkomi Atembelea Banda la PSSSF
Next Article Katibu Mkuu Uchukuzi Aipongeza TASAC,  Kuelimisha Wananchi 
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Katibu Mkuu Uchukuzi Aipongeza TASAC,  Kuelimisha Wananchi 
Habari June 22, 2026
Mkomi Atembelea Banda la PSSSF
Habari June 22, 2026
PSSSF Yapongezwa kwa Kutoa Elimu ya Hifadhi ya Jamii Wiki ya Utumishi wa Umma
Habari June 22, 2026
PDPC  Yashauriwa Kutoa Elimu Kuhusu Taarifa Binafsi 
Habari June 22, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?