MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: WRRB YATOA FURSA MPYA KWA WAFUGAJI NCHINI
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > WRRB YATOA FURSA MPYA KWA WAFUGAJI NCHINI
Habari

WRRB YATOA FURSA MPYA KWA WAFUGAJI NCHINI

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imesema matumizi ya Mfumo wa Stakabadhi za Ghala katika sekta ya mifugo yataimarisha masoko na kuongeza ushindani wa bei ya bidhaa hiyo nchini.
Akizungumza Juni 19, 2026 katika Maonesho ya Mifugo na Mnada wa Kimataifa yanayofanyika katika Shamba la Mbogo, Chalinze mkoani Pwani, Afisa Ubora wa WRRB, Anatolius Kabyemera, amesema bodi hiyo imeingia kwenye sekta hiyo kwa lengo la kuwawezesha wafugaji kuuza mifugo yao kupitia mfumo rasmi na wenye tija.
Habari Picha 12466
Amesema mfumo huo utasaidia wafugaji kuimarisha ufugaji na kuongeza kipato chao ambapo mifugo itahifadhiwa kwenye eneo maalumu lililosajiliwa  kama ghala ya mifugo wakati wakisubiri mnada.
“Mfumo huu utawezesha mifugo kuletwa kwenye ghala ambalo ni eneo teule lenye maji, malisho na wataalamu wa mifugo,  litahesabika kuwa ghala la mifugo. Baada ya mfugaji kuingiza mifugo yake katika ghala akisubiri mnada, atapatiwa stakabadhi itakayomwezesha kupata mkopo kupitia taasisi za fedha ambazo  tumeshaingia nazo makubaliano, kwa mfano NBC,” amesema Kabyemera.
Kwa upande wake, mmoja wa wafugaji waliotembelea banda la WRRB katika maonesho hayo, Moringe Gasper, ameipongeza bodi hiyo kwa kutoa elimu kuhusu matumizi ya mfumo huo katika sekta ya mifugo.
Habari Picha 12467
Amesema wafugaji wengi wako tayari kuona utekelezaji wa mfumo huo unaanza haraka ili nao waweze kunufaika kama ilivyo kwa wakulima wanaotumia mfumo wa stakabadhi za ghala kwa sasa.

You Might Also Like

Apongeza watumishi kwa kutoa huduma bora kwa walimu

Usafirishaji Wa Mizigo SGR Mbioni Kuanza

Mbunge Ataka Vijiji Vinavyozunguka Mlima Kilimanjaro Kulipwa Fedha Za Uwajibikaji

MNH Kuvuna Mifupa Kutengeneza Taya

Wenye Ulemavu Wa Ngozi Wakumbukwa Kupitia FDH, Wapewa Msaada Wa Milioni 20

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mfumo Wa  PPAA Waongeza Ufanisi  Kusimamia Malalamiko Ya Zabuni
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mfumo Wa  PPAA Waongeza Ufanisi  Kusimamia Malalamiko Ya Zabuni
Habari June 19, 2026
TBA Yakaribisha Wawekezaji Kushirikiana  Kwenye  Miradi Ya Ujenzi
Habari June 19, 2026
TOSCI Inatoa Elimu Ya Kufahamu Mbegu Bandia
Habari June 19, 2026
Jua Namba Zako Okoa Maisha Yako
Habari June 19, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?