MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Waziri Kijaji: Huduma ya Kudungwa na Nyuki Kuongeza Kinga Yavutia Bungeni
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Waziri Kijaji: Huduma ya Kudungwa na Nyuki Kuongeza Kinga Yavutia Bungeni
Habari

Waziri Kijaji: Huduma ya Kudungwa na Nyuki Kuongeza Kinga Yavutia Bungeni

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Ashatu Kijaji amesema huduma ya kudungwa na nyuki kwa ajili ya kuongeza kinga ya mwili ni moja ya vivutio vinavyopatikana katika maonesho yaliyoandaliwa na wizara hiyo kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma.

Dkt. Kijaji amesema hayo baada ya kutembelea mabanda mbalimbali ya maonesho pamoja na wabunge wengine mara baada ya kuwasilisha hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa mwaka wa fedha 2026/2027 bungeni.

Amesema maonesho hayo yanalenga kuwaonesha wabunge na wananchi vivutio vya utalii pamoja na huduma mbalimbali zinazopatikana nchini, zikiwemo zinazotokana na mazao ya nyuki.

Habari Picha 12073

“Tunawaonyesha watu kwa vitendo vivutio mbalimbali tulivyobarikiwa navyo ndani ya taifa letu. Hata huduma ya kudungwa na nyuki kwa ajili ya kuongeza kinga ya mwili inapatikana hapa,” amesema Dkt. Kijaji.

Aidha, amesema ongezeko la watalii kwa asilimia 10.2 ni matokeo ya juhudi kubwa zinazofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan katika kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia kampeni mbalimbali za utalii.

Kwa mujibu wa Waziri huyo, maonesho hayo pia yanalenga kuwafanya wabunge kuwa mabalozi wa utalii katika majimbo yao kwa kuwahamasisha wananchi kutembelea vivutio vya ndani ili kuongeza idadi ya watalii wa ndani.

Habari Picha 12074

“Tunataka wabunge wakawe mabalozi wazuri wa kueleza wananchi kuhusu vivutio tulivyonavyo na umuhimu wa kuendeleza utalii wa ndani,” amesema.

Dkt. Kijaji amesema wizara hiyo imewasilisha utekelezaji wa ahadi ilizotoa mwaka 2025 kwa kuonyesha kwa vitendo mafanikio yaliyopatikana katika sekta hiyo.

Ameongeza kuwa katika banda la Bodi ya Utalii Tanzania ( TTB), kuna teknolojia maalumu inayomwezesha mtu kuona wanyama waliopo porini na maeneo mbalimbali ya utalii ikiwemo Ngorongoro Conservation Area, jambo lililowavutia wengi waliofika kwenye maonesho hayo.

Habari Picha 12075

You Might Also Like

AU yataka vyombo vya habari Afrika, kulinda Uhuru wa vyombo vya habari 

Katambi Aitaka TIRDO Kuongoza Mapinduzi ya Kufufua Viwanda Nchini

Wahamasika Kutumia Mbegu Bora Za Karanga Zilizofanyiwa Utafiti Na TARI

Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi

Spika Zungu Atangaza Kifo Cha Mbunge Wa Peramiho, Jenista Mhagama

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Serikali  Kutumia Fursa  ya AFCON,  Miss World Na IPU Kukuza Utalii Nchini
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Serikali  Kutumia Fursa  ya AFCON,  Miss World Na IPU Kukuza Utalii Nchini
Habari May 15, 2026
TFS Yavunja Rekodi Utalii Wa Misitu,Mapato Yapaa Kwa Asilimia 43
Habari May 15, 2026
Serikali Kuimarisha Uvuvi Bahari Kuu Kupitia TAFICO
Habari May 14, 2026
TPHPA Yaimarisha Mapambano Dhidi Ya Visumbufu Vya Mazao
Habari May 14, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?