MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mbunge Ngorongoro Aiomba Serikali Kufungua Uchumi Loliondo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mbunge Ngorongoro Aiomba Serikali Kufungua Uchumi Loliondo
Habari

Mbunge Ngorongoro Aiomba Serikali Kufungua Uchumi Loliondo

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: MBUNGE wa Jimbo la Ngorongoro, Yanick Ndoinyo, ameiomba Serikali kuongeza uwekezaji katika Wilaya ya Ngorongoro, hususan eneo la Loliondo, kwa kufungua miundombinu ya usafiri itakayochochea ukuaji wa uchumi na maendeleo ya wananchi.
.
Ametoa ombi hilo alipokuwa akichangia hotuba ya Wizara ya Uchukuzi bungeni, ambapo amepongeza mafanikio makubwa yaliyopatikana katika sekta za bandari, reli, usafiri wa anga pamoja na miundombinu mingine ya usafirishaji.
Ndoinyo amesema Loliondo ni eneo lenye fursa kubwa za kiuchumi lakini bado halijatumika ipasavyo kutokana na ukosefu wa miradi ya kimkakati.
Ameeleza kuwa bila uwekezaji mkubwa katika sekta ya usafiri, wananchi wa eneo hilo hawataweza kunufaika kikamilifu na kasi ya maendeleo inayotekelezwa nchini chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan.
Mbunge huyo ameisisitiza Wizara ya Uchukuzi kuujumuisha Uwanja wa Ndege wa Waso katika mipango ya maendeleo ya wizara hiyo, akisema uwanja huo una umuhimu mkubwa kwa Wilaya ya Ngorongoro ambayo hadi sasa bado haina barabara za lami.
Amesema kukamilika kwa uwanja huo kutasaidia kuongeza ajira kwa vijana, kukuza biashara na kuimarisha sekta ya utalii kwa kuwa eneo la Waso ni kitovu muhimu kinachounganisha vivutio vya utalii vya Serengeti, Ngorongoro na Ol Doinyo Lengai.
Ndoinyo amesema uwepo wa uwanja huo utafungua uchumi wa Ngorongoro na kuifanya wilaya hiyo kuwa kitovu muhimu cha utalii na biashara,
Huku akisisitiza kuwa anaunga mkono hoja ya Wizara ya Uchukuzi kwa kuwa inalenga kuleta mageuzi makubwa katika uchumi wa Tanzania.

You Might Also Like

Polisi Dar Wakamata Magari 15  Yasiyo na Usajili Rasmi

Wizara ya Maji Yawasilisha Vipaumbele 2026/2027 kwa Bajeti ya Trilioni 1.2

Senene Waongezewa Thamani UDSM

Walimu Ni Nguzo ya Maadili na Uzalendo kwa Taifa – Rais CWT

Sierra Leone Yaipongeza TARURAUjenzi Wa Madaraja, Barabara Za Mawe

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TMA Yakamilisha Ufungaji Mitambo Ya Uangalizi Mpanda, Pemba
Next Article TPHPA Yaimarisha Mapambano Dhidi Ya Visumbufu Vya Mazao
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

TFS Yavunja Rekodi Utalii Wa Misitu,Mapato Yapaa Kwa Asilimia 43
Habari May 15, 2026
Serikali Kuimarisha Uvuvi Bahari Kuu Kupitia TAFICO
Habari May 14, 2026
TPHPA Yaimarisha Mapambano Dhidi Ya Visumbufu Vya Mazao
Habari May 14, 2026
TMA Yakamilisha Ufungaji Mitambo Ya Uangalizi Mpanda, Pemba
Habari May 13, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?