MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mwigulu: Wavivu, Wazembe, Wala Rushwa Serikalini Jiandaeni Na Fyekeo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mwigulu: Wavivu, Wazembe, Wala Rushwa Serikalini Jiandaeni Na Fyekeo
Habari

Mwigulu: Wavivu, Wazembe, Wala Rushwa Serikalini Jiandaeni Na Fyekeo

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: WAZIRI Mkuu Mwigulu Nchemba, ametoa onyo kali kwa watumishi wa umma wazembe, wavivu, wala rushwa na wenye lugha mbaya kwa wananchi, akisisitiza kuwa serikali haitavumilia tabia hizo na ipo tayari kuchukua hatua kali dhidi yao.
Mwigulu ameyasema hayo leo Alhamisi, Novemba 13, 2015 bungeni jijini Dodoma alipokuwa akitoa  shukurani baada ya kuthibitishwa na Bunge kufuatia uteuzi wa Rais Samia Suluhu Hassan wa kuwa Waziri Mkuu.
“Nawaambia watumishi wote wa umma wavivu, wazembe, wala rushwa na wenye lugha chafu kwa wananchi tuwe tayari. Nitakuja na fyekeo na rato,” amesema Waziri Mkuu Mwigulu mara baada ya jina lake kuthibitishwa rasmi na Bunge kuwa Waziri Mkuu.
Habari Picha 10289
Amesema serikali yake itaweka mkazo mkubwa katika kuhakikisha watanzania wote, hasa wale wa kipato cha chini, wanasikilizwa na kuhudumiwa kwa nidhamu katika kila ofisi ya umma.
“Niwahakikishie Watanzania kila aliye Mtanzania, nchi hii ni yake. Watumishi wa umma watalazimika kwenda kwa wananchi kutatua kero zao badala ya wananchi kufuata ofisini,” amesema.
Pia Mwigulu amesema serikali itashirikiana kwa karibu na wananchi kupitia mapendekezo na hoja mbalimbali, akibainisha kuwa kila sauti, hata ya wachache, itasikilizwa kwa usawa kwa sababu Bunge lililopo ni bunge makini lenye dhamira ya kweli ya kuhudumia Watanzania wote..
Katika hotuba yake, Waziri Mkuu huyo amewashukuru wabunge kwa kuthibitisha jina lake kushika nafasi hiyo, pamoja na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kumpendekeza, akiahidi kufanya kazi kwa bidii, uaminifu na juhudi kubwa.
“Majukumu haya si mepesi. Lakini naamini tutayatekeleza yote kama tutamtanguliza Mungu na kuilinda amani ya taifa letu,” amesema.

You Might Also Like

Wanawake Wang’aa Mchakato Uchaguzi Mkuu 2025

Kamati Ya Bunge Yaridhishwa Na Utaratibu Wa Manunuzi Ya Bando

Mfumo Wa KieletronikiWa Albino Kurahisisha Kuwatambua – Ridhiwani

Muhogo, viazi kuongezewa tija kwenye uzalishaji

Wanawake 1,063 Wahitimu Mafunzo Ya Ujuzi VETA Mbeya Kupitia Mpango Wa Rais Samia

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mwalunenge Kuunganisha Mbeya Mjini, Kusukuma Maendeleo Na Ajira Kwa Vijana
Next Article TTCL Yazindua Kifurushi Cha Huduma Tatu Muhimu  
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Habari November 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?