MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mwalim: Niko Tayari Kushirikiana na Majaliwa Nikipewa Ridhaa ya Urais
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mwalim: Niko Tayari Kushirikiana na Majaliwa Nikipewa Ridhaa ya Urais
Habari

Mwalim: Niko Tayari Kushirikiana na Majaliwa Nikipewa Ridhaa ya Urais

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
LINDI: MGOMBEA urais wa Chama Cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalim, amesema yuko tayari kushirikiana na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa endapo atapewa ridhaa na Watanzania katika uchaguzi wa Oktoba 29 mwaka huu 2025.
Habari Picha 10006
Akizungumza na wananchi wa Ruangwa mkoani Lindi, Mwalim amesema hawezi kumdharau Waziri Mkuu Majaliwa kwa kuwa amelitumikia taifa kwa miaka 10.
“Nitakapokuwa Rais nitafanya naye kazi Mzee Majaliwa. Nitalinda heshima na maslahi yake kama Waziri Mkuu. Huyu mzee atakuwa mshauri wangu, hata katika safari za nje nitamwomba twende pamoja maana ana uzoefu mkubwa,” amesema Mwalim.
Aidha, Mwalim ameahidi kuboresha maslahi ya watumishi wa umma kulingana na mazingira ya kazi zao.
“Angalieni polisi wetu wanavyofanya kazi vizuri. Tangu nimeanza kampeni nawapongeza kwa ushirikiano mzuri,” amesema.
Ameongeza kuwa serikali ya CHAUMMA itashirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama bila kufanya mabadiliko ya haraka katika uongozi.
“Sina IGP mwingine, ma-RPC, DC wengine—nitafanya kazi nao hawa hawa. Wanafanya vizuri tutawapongeza, wakikosea tutawakosoa,” amesema.
Mwalim amewataka wananchi wa Ruangwa kuwachagua viongozi watakaowatetea, si kwa misingi ya vyama.
“Msiende kuchagua chama, chagueni mtu atakayesema shida zenu. Nani amewahi kuona Mzee Majaliwa akivaa nguo za chama bungeni? Ndani ya Bunge hakuna mwenyekiti wa chama, hakuna katibu mkuu, bali wabunge wanaowakilisha wananchi wao.
“Msisubiri tena ‘iyena iyena, tieni tieni’ mkidhani chama kitawaletea barabara au bei nzuri ya korosho. Chagueni watu watakaowapigania kweli,” ameseama
Habari Picha 10007
Kwa upande wake, mgombea ubunge wa Jimbo la Ruangwa kupitia CHAUMMA, Njalila Ally, amesema pamoja na changamoto za kiuchumi, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amefanya mambo mengi mazuri ya kukumbukwa.
“Waziri Mkuu Majaliwa amefanya kazi kubwa na tutamkumbuka, ikiwemo kuanzisha timu ya Namungo,” amesema Njalila.

You Might Also Like

Kima Cha Chini Cha Mshahara Chapanda Kwa Asilimia 35.1-Rais Samia

TARI Yaleta Mapinduzi Kilimo cha Minazi

Tume ya Kurekebisha Sheria Yaelimisha Umma Kuhusu Haki za Wanyama

Tanzania Ina Utolevu Wa Chakula Kwa Miaka Minne Uongozi Wa Samia

Mama Janeth Magufuli Atembelea Banda La Ofisi Ya Waziri Mkuu Sabasaba

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article MOI Kuendesha Kambi Maalum Ya Uchunguzi,  Ushauri Wa Kitabibu Kwa Wazee
Next Article Dkt. Mpango: Tumuige Nyerere kwa Kulinda Amani, Uhuru na Maadili ya Taifa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mbunge Asisitiza Sheria za Majiko Safi Ili Kulinda Mazingira
Habari February 3, 2026
Mwalunenge: Bila Rasilimali Watu Na Mtaji, Mipango Ya Kilimo Haitafanikiwa
Habari February 3, 2026
Gulamali Ahoji Bungeni Changamoto ya Mawasiliano Ilongelo
Makala February 3, 2026
Serikali Yaendelea Kuimarisha Uhuru wa Mahakama – Nchimbi
Habari February 2, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?