Na Lucy Lyatuu,Dodoma
WABUNGE ‘wameijia’ juu bajeti ya wizara ya ujenzi wakitaka iwe na mageuzi makubwa ya ujenzi na upanuzi wa barabara mbalimbali nchini pamoja na kuitaka serikali kulipa madeni ya wakandarasi ambayo yamekuwa ni tatizo.
Wabunge wamesema hayo jijini hapa wakati wakichangia bajeti ya wizara ya ujenzi, ambapo kwa kiwango kikubwa wameitaka serikali kuipa fedha wizara hiyo ili ikamilishe miradi yake mbalimbali ya ujenzi wa barabara nchini.

Akizungumza Mbunge wa Mbagala, Burchard Kakuru ameshauri barabara za jiji
A Dar es Salaam kupanuliwa zaidi kwa kuwa msongamano hauwezi kumalizwa bila kuwa na mageuzi makubwa.
Amesema Dar es Salaam ni jji la kibiashara na siku hadi siku msongamano umeendelea kuwepo akitolea mfano eneo la Mbagala,kuwa ziwepo hatua za makusudi kupata suluhu.
Mbunge wa Kiwani,Hijja Hassan Hijja ametaka serikali kkubeba dhamanamyam kulipa fedha za madeni ya wakandarasi kwa kuwa wana madeni mengi na wanahitajimkulipwa kuendelea na ujenzi.
Ameongeza kuwa pia fedha za mfuko wa barabara zilindwe,kuwezesha barabara nyingi kujengwa nchini.

Mbunge wa Musoma Mjini, Mgore Miraji ameitaka serikali kuipa fedha wizara ya ujenzi ili barabara nchini zijengwe pamoja na utekelezaji wa uboreshwaji wa miundombinu.
“Ni kweli barabara zi ahitajika,lakini serikali ipeleke fedha ili zikamilishwe kwa kuwa wizara hiyo inapumulia mashine,” amesemq na kutaka fedha za mfuko wa barabara ziachwe zijenge barabara.
Kwa upande wake Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Kasheku amewashauri wabunge kupitisha bajeti hiyo ambayo imekuwa na mvutano kwa kila mbunge kukumbuka barabara za maeneo walikotoka .

Alisema wizara hiyo haina fedha , ambapo ni muhimu serikali kuipatia fedha ili iweze kuendelea kukamilisha shughuli za ujenzi.

