
Na Lucy Lyatuu, Dodoma
MAMLAKA Ya Elimu Na Mafunzo Ya Ufundi Stadi ( VETA) imesema imeondoa suala la uvaaji wa sare za chuo kwa wanafunzi wanaosomea ujuzibalimbali katika Mamlaka hizo ili kuwezesha watanzania walio wengi kusoma na kupata elimu.

Mkurugenzi wa VETA, Anthony Kisore amesema hayo wakati akizungumza kuhusu jitihada za ueendelezaji ufundi stadi nchini na fursa kwa vijana.
Kuhusu sare kwa wanafunzi amesema Mamlaka imeamua kuondoa sare ili kuwezesha watu mbalimbali wakiwemo wenye umri tofauti kuweza kuchukua hatua na kupata elimu na ujuzi katika mamlaka hiyo.
Amesema kuondolewa kwa sare katila Mamlaka hiyo hakumaanishi kila mwanafunzi atavaa awezavyo bali upo muongozo wa uvaaji nadhifu kwa kilamoja na wenye kuzingatia maadili.
” Upo muongozo wa mavazi kwamba lazima yawe nadhifu.. Na kwamba hata wakati wa kwenda katika karakana za mafunzo, mwanafunzi atapaswa kuvaa kulingana na somo husika, ” Amesema Kisore na kuongeza kuwa kuondolewa kwa sare lunawavuta wale walioogopa kujiunga na Mamlaka hiyo wakihofia suala la kuvaa sare za chuo.
Amesema pamoja na kuondolewa kwa sare lakini uvaaji sio kwa matakwa ya mwanafunzi nali ni wenye kuwa madhifu na wenye maadili ya mtanzania.
Kuhusu fursa kwa vijana kupitia miradi amesema Mamlaka hiyo inaendesha mradi wa ujasiriamali kwa vijana kwa mustakabali wa chakula na kilimo ambao utanufaisha vijana 5631.
Amesema mradi huo ambao unatoaafunzo bure kwa vijana utafundisha teknolojia ya utengenezaji wa zana za kilimo, lengo ni kuwa na wataalam wa zana hizo na utasaidia pia vijana kupata ajira.
“Hakuna ada wala malipo mengine kwa mafunzo katika mradi huu, kinachotakiwa ni kijana kuwa na muda wa kujifunza na utatekelezwa kupitia VETA Kihonda, Manyara,,Mpanda na Arusha na vyuo hivyo vitatoa mafunzo ya muda mfupi.

