MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Utekelezaji Mradi Mkubwa Wa Maji Mwanza Wafikia Asilimia 35
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Utekelezaji Mradi Mkubwa Wa Maji Mwanza Wafikia Asilimia 35
Habari

Utekelezaji Mradi Mkubwa Wa Maji Mwanza Wafikia Asilimia 35

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Maji Kutiririka Kwa Uhakika Mwanza Kufikia Mwaka 2026
Na Lucy Ngowi
MWANZA: MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA), imesema utekelezaji wa mradi mkubwa wa uboreshaji wa mfumo wa usambazaji wa maji safi jijini Mwanza umefikia zaidi ya asilimia 35 ya ukamilishaji.
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa MWAUWASA, Vivian Temu, ameeleza hayo katika ziara ya waandishi wa habari ya kutembelea miradi hiyo.
Habari Picha 9737
Amesema ujenzi wa matenki matano ya maji yenye uwezo wa kuhifadhi jumla ya lita milioni 31 unaendelea katika maeneo ya Kagera (lita milioni 10), Kisesa (milioni 5), Fumagila (milioni 10), Nyamazobe (milioni 5) na Usagara (milioni 1).
Amesema Mradi huo pia unahusisha ulazaji wa mtandao wa bomba wenye urefu wa kilomita 40.5, ambapo mpaka sasa KM 13.7 tayari zimeshalazwa kutoka katika vituo vya kusukuma maji vinavyojengwa maeneo ya Sahwa na Butimba kuelekea matenki husika.
Habari Picha 9738
“Mradi huu ni muhimu kwa maendeleo ya wakazi wa Mwanza. Tunatarajia kazi ya ulazaji wa bomba kuelekea tenki la Kisesa, ambalo ujenzi wake umekamilika, itakamilika mapema ifikapo Machi 2026,” amesema.
Amesema mradi huo unatarajiwa kukamilika rasmi Desemba 2026, na utakapokamilika, unakadiriwa kunufaisha zaidi ya wananchi 450,000 wa jiji la Mwanza na viunga vyake, hususan wakazi wa maeneo ya pembezoni na yale yenye miinuko mikali ambayo hapo awali yalikuwa na changamoto kubwa ya upatikanaji wa huduma ya maji safi.
Amesema matenki yanayojengwa yamepangwa kupokea maji kutoka kwenye chanzo kipya cha uzalishaji maji cha Butimba, ambacho pia ni sehemu ya mradi huu unaofadhiliwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD – Agence Française de Développement).
Habari Picha 9739
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Amani, Waisa Werema, ambaye eneo lake limepitiwa na mradi huo, ameleza kuridhishwa kwake na utekelezaji wa mradi huo akisema kuwa umesaidia kupunguza kwa kiasi kikubwa tatizo la maji katika jamii yao.
“Tunatoa pongezi kwa serikali na kwa Mkurugenzi wa MWAUWASA, Neli Msuya, kwa ushirikiano na viongozi wa mitaa katika kutatua changamoto pale zinapojitokeza,” amesema Werema.
Mradi huo una lengo la kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji safi, kuongeza uwezo wa hifadhi ya maji, na kupunguza uhaba wa maji kwa wakazi wa Mwanza, hatua ambayo inatarajiwa kuongeza ustawi wa afya, uchumi na mazingira ya wakazi wa jiji hilo kwa ujumla.

You Might Also Like

Tanzania, Belarus Zaanza Ukurasa Mpya wa Ushirikiano wa Kimkakati

VETA Yazalisha Bidhaa 825, Zinauzwa Ndani Na Nje Ya Nchi

CHAUMMA kuanzisha mjadala wa elimu ndani ya siku 100

SUA Chatumia Ngamia Mafunzo Ya Vitendo Kwa Wanafunzi

TPHPA: Toeni taarifa mapema milipuko ya kwelea kwelea, nzige, viwavijeshi vamizi inapotokea

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Rais Dkt Mwinyi Afika Katika Dua ya Kumuombea Rais Mstaafu Wa Awamu Ya Pili
Next Article Mwalim: Ardhi Yetu ni Ufunguo wa Uhuru wa Kiuchumi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Ziwa Ngozi Lavuta Mamia Sabasaba, Wageni Washangazwa Na Ramani Ya Afrika Juu Ya Mlima
Habari July 9, 2026
Shirika La Uzalishaji Mali La Polisi Kujenga Vituo Vya Ukaguzi Wa Vyombo Vya Moto
Habari July 9, 2026
Watumishi 7881 Watakaostaafu 2026/27 Watambuliwa Kupitia Kampeni Ya Tunalipa Jana-PSSF
Uncategorized July 8, 2026
Katambi Apongeza Zimamoto Kwa Uwekezaji Wa Vifaa Vya Kisasa
Uncategorized July 7, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?