MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Serikali Yasema Migogoro Ya Ndoa lliyotatuliwa Imeongezeka
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Serikali Yasema Migogoro Ya Ndoa lliyotatuliwa Imeongezeka
Habari

Serikali Yasema Migogoro Ya Ndoa lliyotatuliwa Imeongezeka

Author
By Author
Share
4 Min Read

Na Lucy Lyatuu

SERIKALI imesema Mwongozo wa Taifa wa Uendeshaji, Usimamizi na Uratibu wa Mabaraza ya Usuluhishi wa Migogoro ya Ndoa umewezesha migogoro ya ndoa iliyotatuliwa imeongezeka kutoka migogoro 12,068 kwa mwaka 2022 hadi migogoro 100,464 June, 2025.

Imesema imeendelea na jitihada za kuimarisha taasisi ya familia na ndoa kupitia Mwongozo wa Taifa wa Uendeshaji, Usimamizi na Uratibu wa Mabaraza ya Usuluhishi wa Migogoro ya Ndoa wa mwaka 2023.

Waziri wa Wizara Ya Maendeleo Ya Jamii, Jinsia Wanawake Na Makundi Maalum, Dkt Dorothy Gwajima amesema hayo Dar es Salaam wakati akizungumzia utekelezaji wa shughuli za maendeleo mbalimbali kwa makundi maalum kwa mwaka 2025/26 katika mkutano ulioandaliwa na Idara ya Habari Maelezo.

Amesema Serikali kwa kushirikiana na Wadau hususani Vikundi vya Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jami (SMAUJATA), Sauti ya Watoto Tanzania (SAWATA), Malezi Bora Network na LEMACHU vimeweza kuibua, kukemea na kutoa elimu kwa jamii kuhusu vitendo vya ukatili.

Aidha, amesema tangu kuanzishwa kwa kampeni hizo jumla ya matukio 799 yameripotiwa na kushughulikiwa.

Dkt Gwajima amesema Serikali inaendelea kutoa huduma ya Malezi ya Kambo na Kuasili kwa ajili ya watoto waliokosa malezi katika ngazi ya familia kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo vifo vya Wazazi, Watoto kutupwa pamoja na kutelekezwa na Wazazi/Walezi.

Amesema takwimu zinaonesha huduma ya malezi ya kambo na kuasili imeongezeka kutoka Watoto 85 (Wavulana 45 na Wasichana 40) mwaka 2022 hadi kufikia watoto 562 (wavulana 279 na wasichana 283) mwaka 2025.

Ametoa wito kwa familia zenye uhitaji wa kutoa huduma ya malezi ya kambo na kuasili kuwasilisha maombi yao kwa Kamishna wa Ustawi wa Jamii kupitia Halmashauri zao.

Kuhusu uwezeshaji kwa wananchi amesema wananchi wanawezeshwa kiuchumi ili kuweza kujiajiri na kujipatia kipato kupitia fursa zilizopo, Serikali inafanya juhudi mbalimbali ya uwezeshaji wananchi kiuchumi ikiwemo kutoa Mikopo yenye Masharti Nafuu kwa Wafanyabiashara Ndogondogo ambao idadi kubwa ni vijana ili kuwawezesha kuimarisha mitaji, kukuza biashara na kuongeza ushiriki wao katika shughuli za kiuchumi.

Ameseme uwezeshaji huo unatekelezwa kupitia Benki ya NMB, inayosimamia utoaji, usimamizi, na urejeshaji wa mikopo hiyo yenye riba ya asilimia saba .

Amesema Kupitia Mikopo hiyo jumla ya wafanyabiashara ndogondogo 4,870 wamenufaika na mikopo yenye thamani ya Sh 9,938,820,000.

Ametoa rai kwa wafanyabiashara ndogondogo kujitokeza na kusajiliwa kwenye mfumo wa Wafanyabiashara Ndogondogo Management Information System (WBN kupitia Maafisa Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri zao.

Aidha Dkt Gwajima amehimiza jamii kutambua kuwa amani ni msingi wa maendeleo na ustawi wa jamii, hivyo, kukosekana kwa amani kunasababisha athari hasi hasa kwa makundi maalum yakiwemo Wazee, Wanawake na Watoto.

Amezitaja athari hizo ni pamoja na: kupotea na uharibifu wa mali na makazi; kuongezeka kwa watu wanaopata ulemavu; kutokea kwa vifo na magonjwa ya mlipuko; kuongezeka kwa vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia; Kuongezeka kwa msongo wa mawazo na kiwewe; na kukosekana kwa huduma muhimu za kijamii kama vile huduma za afya, maji safi na salama, usafiri, umeme na chakula.

Amesema Wizara yake imeanzisha utaratibu kutoa huduma bora zaidi kwa jamii kupitia falsafa mpya ya KAZA KAZAWA (Kasi zaidi, Karibu zaidi na Wananchi).

You Might Also Like

TPHPA yakusanya zaidi ya sampuli 10,000 za mbegu asili

Mgombea Urais CHAUMMA Ahaidi Soko La Kisasa Feri

TARURA Dar Yaendelea Na Ujenzi Wa Miundombinu Ya Barabara Iliyosimama Kutokana Na Mvua

Rais Samia Kushiriki Mkutano Wa Wakuu Wa Nchi Ethiopia

Wanafunzi 431, Watumishi 52 Watembelea TARI kujifunza Kilimo

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Katambi Aagiza Ushindani Wa Haki Ili Kulinda Bei, Walaji
Next Article Wanataaluma Wahimizwa Kutumia Tafiti Kama Chachu ya Mabadiliko ya Jamii
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

CAG Aipongeza TARURA Kwa Ujenzi Wa Miundombinu
Habari January 9, 2026
Tuna Deni La Kusimamia Miradi Na Kusikiliza Kero za wananchi Ili Kuleta Maendeleo Ya Kweli-Salome
Habari January 9, 2026
Rais Dkt Samia Azindua Majengo Ya Kisasa
Habari January 8, 2026
TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar
Habari January 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?