MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Serikali Yaeleza Mikakati Ya Kuwezesha Vijana Katika Soko La Ajira
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Serikali Yaeleza Mikakati Ya Kuwezesha Vijana Katika Soko La Ajira
Habari

Serikali Yaeleza Mikakati Ya Kuwezesha Vijana Katika Soko La Ajira

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: SERIKALI inakabiliana na tatizo la ajira kwa kubuni na kutekeleza programu maalum zinazowawezesha vijana kujifunza kwa vitendo kupitia sekta zinazozalisha ajira kwa wingi.
Sekta hizo ni kilimo kupitia programu ya Jenga Kesho iliyobora (BBT), ujasiriamali, na madini kupitia Programu ya Mining for a better Tommorrow (MBT).
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Ridhiwani Kikwete amesema hayo leo Februari 10, 2025 bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mpendae, Toufiq Turky.
Ridhiwani pia amesema serikali  inafanya maboresho ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 Tolea la Mwaka 2023 ambayo yanasisitiza mafunzo kwa kuandaa wataalamu.
“Kupitia ujenzi wa miundombinu ya Kimkakati muhimu inayochochea uchumi, vijana wameajiriwa na kunufaika na urithishwaji ujuzi kutoka kwa wataalamu wa nje mfano ujenzi wa Bwawa la umeme la Mwalimu Nyerere na barabara za mwendokasi (BRT),” amesema Mhe. Kikwete
Vile vile amesema Serikali itaendelea kubuni na kutekeleza programu ya kukuza ujuzi ambayo inalenga kukuza ujuzi kwa nguvu kazi ili kuwezesha vijana kushindana katika soko la ajira mfano mafunzo ya kuongeza ujuzi kwa wafanyakazi waliopo kazini na kwa wajasiriamali.
Waziri Kikwete amesema mkakati mwingine ni kuweka msisitizo kwenye matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), katika kuzalisha fursa nyingi za ajira kwa vijana.
“Napenda kulihakikishia Bunge lako Tukufu kwamba serikali itaendelea kusimamia na kuhakikisha vijana wanaandaliwa ili wapate ujuzi unaohitajika katika soko la ajira na hivyo kumudu ushindani wa ajira,” amesema.
Turky amehoji kuna mpango gani wa kuwandaa vyema vijana waweze kushindana katika soko la ajira ndani na nje ya Tanzania ili kukabiliana na upungufu wa ajira nchini.
Akijibu swali hilo, Waziri Kikwete ametaja mipango ya serikali katika kuwaandaa vijana ili kumudu ushindani katika soko la ajira ndani na nje ya nchi.

You Might Also Like

Spika Tulia Kufungua Kongamano La Uhuru Wa Wanataaluma Afrika UDSM

Tari Ilonga yaboresha mbegu, mavuno yapanda hadi tani 3.8 kwa hekta

LATRA Yaboresha Mfumo Wa Taarifa Kwa Abiria

Waziri Mkuu Majaliwa Azungumzia Urushaji Wa Satelite Tanzania

Asisitiza Umuhimu Wa Kukamilisha Miradi Kwa Mujibu Kuzingatia Mikataba

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Dendego Achangisha Bilioni 1.7, Ujenzi Ofisi Ya CCM
Next Article Wana Dodoma Wakoshwa Na Uboreshaji Mitaala
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Serikali Yaweka Mkazo Kufufua Viwanda Musoma Ili Kuongeza Ajira
Habari April 24, 2026
Program Ya Mama Samia Ya Kurasimisha Ujuzi Yazinduliwa
Habari April 23, 2026
TEA, Wizara ya Elimu Zanzibar Kushirikiana Kuimarisha Miradi ya Elimu
Habari April 23, 2026
Bajeti Yadhihirisha Uhakika Wa Nishati Nchini
Habari April 23, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?