MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Profesa Kabudi Atoa Maagizo Mazito Bodi Ya Ithibati Ya Waandishi Wa Habari
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Profesa Kabudi Atoa Maagizo Mazito Bodi Ya Ithibati Ya Waandishi Wa Habari
Habari

Profesa Kabudi Atoa Maagizo Mazito Bodi Ya Ithibati Ya Waandishi Wa Habari

Author
By Author
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari imeagizwa kuhakikisha waandishi wa habari wote wanazingatia sheria, kanuni na miongozi inayosimamia taaluma yao ili kudhibiti uandishi usio wa kimaadili na kuongeza heshima ya taaluma hiyo.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Palamagamba Kabudi ameagiza hayo leo Machi 3, 2025 wakati akizindua bodi hiyo mkoani Dar es Salaam.

Kabudi amesema, “Katika hili tunapaswa kuanza kwa kuwalea na kuwapa miongozo mbalimbali juu ya taaluma yao,”.

Agizo lingine aliloagiza bodi hiyo ni  kuandaa na kusimamia utaratibu wa usajili wa waandishi wa habari kwa kuzingatia viwango vya kitaaluma, mfumo ambao unapaswa kuwa shirikishi na unaoendana na maendeleo ya teknolojia na mazingira ya sasa ya sekta ya habari.

Agizo lingine alilollitoa Profesa Kabudi kwa bodi hiyo ni kuhakikisha kuwa waandishi wa habari wanazingatia maadili ya taaluma kwa kutoa miongozo na mafunzo ya mara kwa mara.

Ameiagiza bodi hiyo kushirikiana na vyombo vya habari, vyuo vya mafunzo ya uandishi wa habari, na wadau wengine ili kuhakikisha kuwa waandishi wa habari wanapata mafunzo ya mara kwa mara na kuwa na ujuzi wa kisasa.

Pia ameiagiza kutoa elimu kwa wananchi ili waelewe umuhimu wa ithibati ya waandishi wa habari na jinsi inavyosaidia kuboresha sekta ya habari.

“Katika ulimwengu wa sasa wa kidijitali, Bodi hii inapaswa kusaidia kuhakikisha kuwa waandishi wa habari wanatumia teknolojia kwa manufaa ya taaluma yao bila kuvunja maadili. Hii ni pamoja na kudhibiti matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii katika utoaji wa habari.

“Ikiwa ni pamoja na kushirikiana na mamlaka husika kuhakikisha kuwa waandishi wa habari wanafanya kazi zao kwa usalama bila vitisho, unyanyasaji, au vikwazo visivyo vya lazima. Usalama wa wanahabari ni msingi wa uhuru wa vyombo vya habari,” amesema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Tido Mhando amesema bodi hiyo ni chombo muhimu cha kuhakikisha taaluma ya habari inafuata weledi na ubora unaotakiwa.

Amesema atatekeleza maagizo yote waliyopewa na Waziri Kabudi kwa moyo wa uzalendo, uaminifu na uadilifu.

 

You Might Also Like

Rafiki Mkubwa wa Trump, Elon Musk atanufaika vipi baada ya kumuunga mkono?  

MOI Yaokoa Bilioni 150 Matibabu Ya Kibingwa

Afrika ijadili changamoto sekta ya utalii – UN

Walimu Wanaofundisha Lugha Ya Kichina Tanzania Wakutana

Serikali Yaja Na Kanuni Mpya Ya Sheria Ya Fidia   Kuboresha Mazingira Ya Mfanyakazi 

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article VETA Yapaa Miaka Minne Ya Rais Samia
Next Article Benjamini Mkapa Yapandikiza Mimba 21, Watano Waongezewa Nguvu Za Kiume
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?