Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: MTAFITI kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Priscilla Kaijage amefanya utafiti kuangalia namna mimea ya asili inavyoweza kudhibiti magonjwa ya fangasi kwenye mimea, hususan maharage.
Priscilla ambaye pia ni Mhadhiri Msaidizi chuoni hapo, amesema katika utafiti wake ametumia mimea miwili aina ya mwarobaini na ‘comfrey’ ujulikanao kama CD4 , uliolenga kupunguza matumizi ya dawa za dukani ambazo nyingi zinatoka nchi za nje, ili kupunguza madhara kwenye mazingira.
“Kwenye utafiti nilikuwa na mimea hiyo miwili na pia concentration tofauti. Katika utafiti mwarobaini niliochakata kwa njia ya kawaida ambayo nilisaga kwenye maji ulifanya vizuri zaidi ikilinganishwa na kemikali za dukani.
“Dawa za dukani zinasababisha madhara kwenye mazingira na pia kwa binadamu, watu yaani wanaopiga awa hiyo, wanaokula zile mboga wanapata madhara zinaingia kwenye mwili taratibu lakini baada ya muda kuna tatizo la kansa.
“Tunajaribu kuwa na namna nyingine ambayo ina manufaa kwenye mazingira, binadam, wanyama na wanaotuzunguka,” amesema.
Ametaja malengo yake kuwa na bidhaa ambayo ina manufaa kimazingira na kiafya, pia wakulima watumie waachane na dawa za dukani.