MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mongela Ajiridhisha Ushindi wa Kishindo , Uchaguzi Serikali za Mitaa,Uchaguzi Mkuu CCM
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mongela Ajiridhisha Ushindi wa Kishindo , Uchaguzi Serikali za Mitaa,Uchaguzi Mkuu CCM
Habari

Mongela Ajiridhisha Ushindi wa Kishindo , Uchaguzi Serikali za Mitaa,Uchaguzi Mkuu CCM

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
4 Min Read

Na Mwandishi Wetu

NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, John Mongella amesema baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Chama 2020-2024 amejiridhisha kwamba chama kinaingia katika chaguzi za Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu ujao kwa uhakika wa ushindi wa kishindo.

Akizungumza baada ya kupokea utekelezaji wa Ilani ya CCM mwaka 2020-2024 kutoka Ofisi ya Mkoa wa Shinyanga, Mongella amesema kutokana na utekelezaji mzuri wa ilani chama hicho kina uhakika wa ushindi na kwamba waendelee na kasi ya kuleta maendeleo ili kero zote ziishe.

Mongella ambaye yupo kwenye ziara ya siku saba mkoani Shinyanga kama mlezi wa mkoa huo, pia amewataka viongozi wa ngazi ya mkoa na hadi mitaa kufanya kazi ya kuwaletea maendeleo wananchi.

 

Mongella amesema Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imedhamiria kwa dhati kuboresha maisha ya wananchi ikiwa ni pamoja na kuleta pembejeo za kilimo kwa wakati, na maafisa ugani kutoa elimu kwa wakulima.

Awali akizungumzia kilimo, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anamringi Macha amesema kutokana na mvua nyingi za msimu wa kilimo uliopita, uzalishaji wa zao la pamba umepungua. “Kutokana na mvua nyingi, uzalishaji wa zao la pamba umepungua kwa kiasi kikubwa, lakini mazao mengine kama tumbaku na mpunga uzalishaji ni wa kuridhisha,” amesema

.Amesema kwa sasa serikali imejikita katika kuhakikisha miradi yote iliyoko kwenye ahadi za uchaguzi 2020-2025 inatekelezeka kwa wakati.

Pia, Mongella amesisitiza umuhimu wa vijana kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo, akibainisha kuwa wao ni nguvu kazi ya taifa na wanayo nafasi kubwa ya kuchangia ustawi wa jamii.

Ameesema ni muhimu kwa vijana kujihusisha na kilimo cha kisasa na kutumia teknolojia ili kuongeza tija.

Mongella amepongeza juhudi za serikali katika kutekeleza miradi ya maendeleo, ikiwemo ujenzi wa barabara, hospitali, na shule, na kusema kuwa juhudi hizo zimeongeza imani ya wananchi kwa chama hicho.

 

Amesema kuwa serikali inatekeleza kwa vitendo ahadi zake na kwamba wananchi wanaona mabadiliko.

Katika sekta ya afya, Mongella amesifu serikali kwa kuboresha huduma za afya na kuongeza upatikanaji wa dawa na vifaa tiba katika vituo vya afya.

Amesema hatua hizi zimepunguza vifo vya akina mama na watoto na kuongeza ubora wa huduma zinazotolewa.

Vilevile, ametoa wito kwa viongozi wa afya kuongeza juhudi katika kutoa elimu ya afya kwa wananchi.

Amepongeza jitihada za viongozi wa mkoa katika kupambana na rushwa na ufisadi, akisema kuwa vitendo hivyo vinadhoofisha juhudi za maendeleo.

Mongella amesisitiza umuhimu wa kuwa na viongozi waadilifu na wenye kujali maslahi ya wananchi, na kuwaasa wananchi kuwafichua wale wote wanaojihusisha na vitendo vya rushwa

.Mongella pia amezungumzia umuhimu wa mazingira na alitoa wito kwa wananchi wa Shinyanga kupanda miti na kulinda vyanzo vya maji.

Amesema kuwa suala la uhifadhi wa mazingira ni jukumu la kila mmoja, na kwamba serikali itaendelea kutoa ushirikiano ili kuhakikisha mazingira yanakuwa salama kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Katika ziara yake, Mongella atatemblea Shinyanga Mjini, Kahama, Msalala, Ushetu, Shinyanga Vijijini na kufanya mikutano ya ndani na hadhara.

You Might Also Like

TUCTA: Waajiri Watekeeze Nyongeza Ya Kima cha Mishahara Sekta Binafsi

Wafugaji huchakachua maziwa kwa kuongeza mafuta, maji, magadi au mkojo wa ng’ombe

Zuhura Yunus Atoa Neno Kwa Madereva 

EAC Yaweka Mguu Chini Ushirikishwaji Wa Wanawake Katika Amani, Ulinzi Na Usalama

Balozi Sirro: Bila Amani, Maendeleo Hayapo Kigoma

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wahandisi 428 Wajengewa Uwezo Kukuza Taaluma
Next Article Halmashauri Zahimizwa Kujenga Viwanda Vya Michezo.
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Watendaji Wakuu Waagizwa Kuifanya Dira 2050 Kuwa Mwongozo Wa Maamuzi Yao
Habari July 24, 2026
Nchi za SADC Zahimizwa Kuimarisha Umoja Kukabili Changamoto
Uncategorized July 17, 2026
Wananchi Washauriwa Kutumia  Wataalam Wa Ujenzi Kuepuka Madhara
Habari July 14, 2026
July 14, 2026
Uncategorized July 14, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?