MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: MOI Yazindua Mfumo Mpya Wa Kielektroniki Wa Kupanga Miadi Na Madaktari
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > MOI Yazindua Mfumo Mpya Wa Kielektroniki Wa Kupanga Miadi Na Madaktari
Habari

MOI Yazindua Mfumo Mpya Wa Kielektroniki Wa Kupanga Miadi Na Madaktari

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
DAR ES SALAAM: TAASISI ya Tiba ya Mifupa, Ubongo na Mishipa ya Fahamu Muhimbili (MOI) imezindua rasmi mfumo mpya wa kidijitali wa kuweka miadi na madaktari, ujulikanao kama ‘MOI Online Appointment System’, unaolenga kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wagonjwa kwa njia ya mtandao bila kulazimika kufika hospitalini.
Uzinduzi wa mfumo huo umefanyika lSeptemba 15, mwakq huu 2025, ukiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Dkt. Mpoki Ulisubisya, ambaye amesema kuwa lengo la kuanzishwa kwa mfumo huo ni kupunguza usumbufu kwa wagonjwa na kuondoa msongamano wa watu wanaofika hospitalini kwa ajili ya kupanga miadi.
Habari Picha 9419
“Kwa kutumia mfumo huu, mgonjwa anaweza kuchagua daktari anayemtaka, tarehe, muda pamoja na kliniki anayoihitaji. Hii itaepusha hali ya kufika hospitali na kukuta daktari hayupo au kliniki haifanyi kazi siku hiyo,” amesema Dkt. Mpoki.
Ameeleza kuwa mara baada ya kuweka miadi, mgonjwa atapokea ujumbe mfupi wa maandishi unaothibitisha miadi yake, Endapo daktari atakuwa na udhuru, taarifa hiyo pia itatumwa kwa mgonjwa kupitia simu yake, kumpa fursa ya kuchagua daktari mwingine au kupanga tarehe mbadala.
Mfumo huo unapatikana saa 24 kwa siku, siku saba kwa wiki, kupitia simu janja, kompyuta mpakato au kishikwambi kwa kutumia tovuti rasmi ya taasisi hiyo: www.moi.ac.tz au moja kwa moja kupitia kiunganishi: https://miadi.moi.ac.tz/appointment/. Mgonjwa atatakiwa kujaza taarifa zake binafsi kabla ya kuwasilisha maombi ya miadi.
“Hii ni hatua muhimu katika utoaji wa huduma bora na kwa wakati. Hata hivyo, wagonjwa ambao hawataweza kutumia mfumo huu hawatanyimwa huduma; wote watapokelewa kama kawaida.
“Tofauti ni kwamba mfumo huu unampa mgonjwa uhakika wa kupata huduma kwa muda anaoutaka na kwa daktari anayemchagua,” amesema Dkt. Mpoki.
Amewahimiza Watanzania kutumia mfumo huo mpya, akisisitiza kuwa ni sehemu ya jitihada za taasisi katika kusogeza huduma kwa wananchi kupitia mifumo ya kidijitali, sambamba na mabadiliko ya sayansi na teknolojia.

You Might Also Like

Chinyeli Aahidi Chakula Bure kwa Wazee, Mwanyemba Kupambana Kutafuta Maendeleo

TDB Yaheshimisha Tasnia Ya Maziwa

UDSM,YULHO kujenga kituo cha kupima madini

‘Skills For Their Future’ Yanufaisha Wanafunzi Zaidi Ya 1000, Walimu 64 

Halmashauri Zahimizwa Kujenga Viwanda Vya Michezo.

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wananchi Watakiwa Kufahamu Sheria Na Miongozo
Next Article OCPD Yakabidhi Juzuu Mpya za Sheria kwa Ofisi ya Taifa ya Mashitaka
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Waziri Mkuu Majaliwa Akabidhi Tuzo kwa BoT Geita
Habari September 22, 2025
BoT Yarahisisha Uuzaji wa Dhahabu kwa Wachimbaji, Yatoa Punguzo La Mrabaha
Habari September 22, 2025
Waziri Mkuu Apongeza Huduma Kidijitali za NSSF, Maonesho Ya Madini Geita
Habari September 22, 2025
Mkuu Wa Mkoa Shinyanga Asifu Kazi Ya Bodi Bima Ya Amana
Habari September 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?