MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mkenda: Bunifu Zigeuke Bidhaa Na Biashara
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mkenda: Bunifu Zigeuke Bidhaa Na Biashara
Habari

Mkenda: Bunifu Zigeuke Bidhaa Na Biashara

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, amesema Serikali inaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wabunifu nchini ili bunifu zao zisitumike kama maonesho pekee, bali zigeuke kuwa bidhaa na biashara zitakazochangia uchumi wa Taifa.
Profesa Mkenda ameyasema hayo wakati akifungua rasmi Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu 2026, katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara, jijini Tanga, Agosti 18, 2026.
Amesema Serikali tayari imeshuhudia mafanikio kupitia mashindano ya ubunifu, ambapo baadhi ya bunifu zimeingia sokoni na kuwa chanzo cha kipato kwa wabunifu, zikiwamo mashine ya kukamua mafuta ya parachichi, mabegi ya shule yenye sola, vifaa vya kusaidia wanafunzi wenye ulemavu, teknolojia za usindikaji wa chakula cha mifugo na mita janja za maji.
Amesema Serikali inafuatilia takribani bunifu 70 katika hatua mbalimbali za maendeleo na inaendelea kushirikiana na taasisi na sekta binafsi kuzisaidia kufikia hatua ya kibiashara.
“Lengo ni kuhakikisha bunifu hazibaki kwenye maonesho pekee, bali zinakuwa bidhaa zinazotumika na kuleta matokeo kwa jamii na uchumi,” amesema.
Aidha, amesema hadi sasa halmashauri 90 zimeanzisha Madawati ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu, huku Serikali ikiwa na mpango wa kuyafikisha katika halmashauri zote nchini. Serikali pia, kwa kushirikiana na Benki ya CRDB, imeweka utaratibu wa kuwasaidia wabunifu kupata mitaji, huku ikiendelea kushirikiana na Watanzania wanaoishi nje ya nchi kutafuta masoko, utaalamu na fursa za uwekezaji.
Katika hatua nyingine, Ofisa Uhusiano Mwandamizi kutoka Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim (CFR), Maryciana Mhagama, amesema Diplomasia ya Uchumi ya Serikali ya Tanzania inalenga kuimarisha nafasi ya nchi kiuchumi kwa kutumia fursa mbalimbali zinazotokana na ushirikiano wa uwili, kikanda na kimataifa, hususan maeneo huru ya biashara barani Afrika.
Mhagama ameyasema hayo katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara, Tanga, ambako CFR ni miongoni mwa taasisi zinazoshiriki katika Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu.
“Pamoja na mambo mengine, Uhusiano wa Kimataifa umeweka msisitizo katika Diplomasia ya Uchumi, Uwekezaji, ukuaji wa Biashara, Mikutano, Utamaduni na Utalii. Kwa kuzingatia fursa zilizopo, Tanzania inaendeleza Diplomasia ya Uchumi katika Uhusiano wa Uwili, Kikanda na Kimataifa,” amesema Mhagama.
Akizungumzia mafunzo yanayotolewa na Kituo hicho, amesema kinaendelea kuwaandaa vijana wa Kitanzania kuwa mahiri na wenye weledi kitaaluma, wazalendo na raia wema wenye utayari wa kutoa mchango kwa Taifa.
Amesema Kituo kinatoa mafunzo na kozi mbalimbali katika masuala ya Uhusiano wa Kimataifa, Diplomasia, Menejimenti ya Uhusiano wa Kimataifa, Utawala wa Kimkakati na Diplomasia ya Uchumi.
Mhagama amesema Kituo kimeandaa mafunzo kuhusu Diplomasia, Itifaki na Ustaarabu, “Diplomacy, Protocol and Etiquette”, yatakayofanyika kuanzia Agosti 24 hadi 28, 2026, CFR, Dar es Salaam, akiwataka wadau kutoka taasisi za umma na sekta binafsi kutumia fursa hiyo.
Wiki hiyo yenye kaulimbiu “Elimu, Ujuzi na Ubunifu: Njia ya Kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050” inaendelea hadi Agosti 24, 2026.

You Might Also Like

TAKUKURU, Manispaa Ubungo Yawafikia Waendesha Bajaji, Bodaboda

TALGWU Taifa Yataja Kero Saba Kubwa za Watumishi wa Serikali za Mitaa

Trump Amteua Mtendaji Mkuu White House, Safari Ya Kuunda Timu Yake

SGR Kipande Cha Saba Na Nane kuanza kujengwa

NIT Yasema Ina Uwezo Wa Kufundisha Kozi Ya Urubani

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Barabara Zinazopasuka, Suluhisho Linalotoka Maabara za Tanzania
Next Article Miaka 40 ya COSTECH: Teknolojia Yafungua Milango ya Elimu kwa Wasioona
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Miaka 40 ya COSTECH: Teknolojia Yafungua Milango ya Elimu kwa Wasioona
Makala August 20, 2026
Barabara Zinazopasuka, Suluhisho Linalotoka Maabara za Tanzania
Makala August 19, 2026
Mnyama Check App: Ubunifu Wamtoa Mfugaji Gizani hadi Kidijitali
Makala August 18, 2026
Waziri Mkenda Kuzindua Wiki Ya Elimu,Ujuzi Na Ubunifu,Washiriki Takriban 300 Waonesha Bunifu Mbalimbali
Habari August 17, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?