MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mkenda Atoa Tuzo kwa Waajiri Wanaowasilisha Michango kwa Wakati
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mkenda Atoa Tuzo kwa Waajiri Wanaowasilisha Michango kwa Wakati
Habari

Mkenda Atoa Tuzo kwa Waajiri Wanaowasilisha Michango kwa Wakati

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Mwandishi Wetu
MWANZA: WAZIRI  wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda amekabidhi tuzo kwa waajiri wanaowasilisha kwa wakati michango ya wafanyakazi wao katika Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), ikiwa ni sehemu ya kutambua uadilifu na uwajibikaji wao katika kulinda haki za wafanyakazi.
Mkenda amekabidhi tuzo hizo katika Mkutano Mkuu wa Umoja wa Wanawake Wamiliki wa Shule na Vyuo vya Kati Tanzania (TAWOSCO), ambapo NSSF pia ilitoa elimu kuhusu hifadhi ya jamii na maboresho ya huduma mbalimbali, hasa katika matumizi ya mifumo ya kidijitali.
Kwenye mkutano huo, Mkenda ametoa pongezi kwa TAWOSCO kwa mchango wao kwenye maendeleo ya elimu nchini, huku akimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa mageuzi makubwa yanayoendelea kushuhudiwa katika sekta hiyo, hasa uboreshaji wa miundombinu na upanuzi wa fursa za elimu.
“Tunatambua mchango mkubwa wa sekta binafsi, hususan wanawake wamiliki wa shule, katika kutoa ajira na kukuza elimu.
“Kwa kutambua hilo, leo tunatambua pia waajiri waaminifu wanaotekeleza wajibu wao kwa wafanyakazi kupitia NSSF,” amesema.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Saidi Mtanda amewapongeza wanawake wa TAWOSCO kwa juhudi zao katika kutoa elimu, akisisitiza kuwa mchango wao ni nyenzo muhimu ya maendeleo ya taifa.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba, Meneja wa Uandikishaji, Ukaguzi na Matekelezo, Cosmas Sasi amesema hadi sasa, wanachama 131 wa TAWOSCO sawa na asilimia 66 wamejiunga rasmi na NSSF, na kati yao, wanachama 35 wanatekeleza kikamilifu wajibu wa kuchangia michango kila mwezi.
Amesisitiza kuwa kuna haja kwa wanachama wenye malimbikizo kuwasiliana mapema na ofisi za NSSF ili kuweka mipango ya ulipaji, badala ya kusubiri hatua za kisheria ambazo zinaweza kuepukika kwa mawasiliano ya karibu.
Akizungumzia maboresho ya huduma, Sasi ameeleza kuwa NSSF imeongeza ufanisi kwa kuanzisha mifumo ya kidijitali ikiwemo NSSF Portal, NSSF App, WhatsApp Chatbot, pamoja na huduma za USSD na SMS, zinazowawezesha wanachama na waajiri kupata huduma nyingi bila kufika ofisini.
Katika risala yao, Makamu Mwenyekiti wa TAWOSCO, Christa Rweyemamu ameeleza kuwa umoja huo una wanachama 195 wanaohudumia zaidi ya wanafunzi 900,000 na kutoa ajira kwa zaidi ya watu 5,000 nchini.
Ametoa shukrani kwa NSSF kwa kushiriki na kusaidia kuwajengea uwezo wanachama kuhusu masuala ya hifadhi ya jamii.

You Might Also Like

Samia: Sera Iliyozinduliwa, Somo La Ujasiriamali Ni Lazima

Ridhiwani: Ili Kufikia Muafaka Masuala Ya Kazi, Serikali Inahimiza  Vyombo Vya Mashauriano

TMDA Kudhibiti Bidhaa Za Tumbaku Ili Wananchi Wasiendelee Kupata Madhara

Askari wa Jeshi La Uhifadhi Kusini Wakumbushwa Wajibu

USCAF Yawapatia Mafunzo Ya TEHAMA Walimu 1585

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Majaliwa Aomba Watanzania Wapatiwe Mafunzo Belarus Kuendeleza Kilimo
Next Article Samia Mgeni Rasmi Siku Ya Mashujaa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Tume Ya Ulinzi Wa Taarifa Binafsi Yatoa Siku Saba Kwa Taasisi Kujisajili
Habari June 12, 2026
Teknolojia Ya Juisi YA Ndizi Kali Yafungua Fursa Mpya Za Viwanda, Ajira
Makala Uncategorized June 12, 2026
Serikali Yaingia Makubaliano Ya Ushirikiano Na DIT Kuimarisha Usimamizi Wa Mataifa
Habari June 8, 2026
Wananchi Waelimishwa Masharti ya Kubadilisha Noti Zilizochakaa, Kuungua na Kuchanika
Habari June 7, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?