MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mbunge Majule ataka wanawake wapewe elimu ya fedha na mitaji
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mbunge Majule ataka wanawake wapewe elimu ya fedha na mitaji
Habari

Mbunge Majule ataka wanawake wapewe elimu ya fedha na mitaji

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: MBUNGE wa Viti Maalum, Dkt. Neema Majule, ameitaka Serikali kuimarisha uwezeshaji wa wanawake kwa kuwapatia elimu ya fedha, ujasiriamali na mitaji ili waweze kushiriki kikamilifu katika kukuza uchumi wa nchi.
Akichangia hotuba ya Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, bungeni Dodoma, Dkt. Majule amesema wanawake wanahitaji zaidi ya motisha; wanapaswa kufundishwa namna ya kubuni na kuendeleza mawazo ya biashara pamoja na kupata mifumo rahisi ya kuwasaidia kuanzisha na kukuza miradi yao.
Amepongeza mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, akieleza kuwa katika kipindi cha miaka minne, sekta ya elimu imepiga hatua kubwa kutokana na ujenzi wa madarasa zaidi ya 78,000 na shule nyingi za kisasa hata vijijini.
Amesema hatua hiyo imeondoa changamoto ya wanafunzi kusoma katika mazingira duni.
Aidha, ameisifu Serikali kwa kuboresha sekta ya afya kwa kujenga zahanati katika vijiji, vituo vya afya, hospitali za wilaya, mikoa na rufaa, pamoja na kuimarisha upatikanaji wa vifaa tiba.
Kuhusu uchumi, amesema Tanzania inaendelea kupiga hatua kuelekea uchumi wa kati wa juu, lakini amesisitiza umuhimu wa uchumi shirikishi unaowahusisha wanawake na wanaume katika sekta zote, ikiwemo kilimo na sekta binafsi.
“Maendeleo haya hayawezi kuwa endelevu bila ushiriki wa wanawake. Wanawake washirikishwe kuanzia kupanga, kutekeleza hadi kutathmini miradi ya maendeleo,” amesema.
Dkt. Majule amesisitiza umuhimu wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri, akitaka usimamizi na ufuatiliaji wake uimarishwe ili kuhakikisha wanawake wananufaika ipasavyo.
Pia amezungumzia Sh. Bilioni 200 zilizotengwa kwa ajili ya wajasiriamali, akitaka ziwanufaishe walengwa kwa kuwepo utaratibu mzuri wa utoaji wake.
Ameongeza kuwa pamoja na mitaji, wanawake wanahitaji masoko ya uhakika ya bidhaa zao, hivyo akashauri kuwepo mifumo ya kuwaunganisha na masoko ya ndani na nje ya nchi ili kuongeza tija na kipato.

You Might Also Like

TPHPA Yazidisha Ulinzi wa Mazao, Kudhibiti Magonjwa ya Viazi, Funza Weupe

Majaliwa Aipongeza TPHPA kwa Kuhakikisha Usalama wa Chakula Nchini

Naibu Waziri Katambi Asisitiza Ufanisi na Ubunifu Kwenye SIDO

UDSM Yabuni Teknolojia Mpya ya Kuhesabu Samaki Kwa Haraka 

TEITI Yashiriki Maonesho ya Nane ya Uwekezaji Sekta ya Madini Geita

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mbunge Msita Ataka Ukarabati Wa Haraka Barabara Zilizoharibiwa Na Mvua
Next Article Waziri Ulega aridhishwa na miradi ya dharura TANROADS
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Ubunifu Wa Majengo Watakiwa Kuzingatia Tija Na Gharama Nafuu
Habari April 11, 2026
Waziri Ulega aridhishwa na miradi ya dharura TANROADS
Habari April 11, 2026
Mbunge Msita Ataka Ukarabati Wa Haraka Barabara Zilizoharibiwa Na Mvua
Habari April 11, 2026
Mbunge Ndoinyo Aitaka Serikali Kugawa Ngorongoro Kusogeza Huduma Karibu
Habari April 10, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?