MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mbegu Bora za Miwa Zenye Tija ya Tani 200 kwa Hekta Zaendelea Kuwanufaisha Wakulima
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mbegu Bora za Miwa Zenye Tija ya Tani 200 kwa Hekta Zaendelea Kuwanufaisha Wakulima
Habari

Mbegu Bora za Miwa Zenye Tija ya Tani 200 kwa Hekta Zaendelea Kuwanufaisha Wakulima

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
MOROGORO: MBEGU bora za miwa zinazozalishwa na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) Kibaha mkoani Pwani, zinaendelea kuwa na mchango mkubwa kwa wakulima na viwanda kutokana na uwezo wake wa kutoa tija kubwa, ikiwemo kuvuna hadi tani 200 kwa hekta.
Mtafiti kutoka TARI Kibaha, Msajigwa Mwakyusa, amesema hayo katika maonesho ya nanenane  Kanda ya Mashariki yanayoendelea mkoani Morogoro.
Amesema kuna makundi mawili ya mbegu za miwa zinazotegemea umwagiliaji na zile zinazotegemea mvua.
“Kwa wakulima wa nje, kuna mbegu sita zinazotumika ambazo ni TARSCA 1, TARSCA 2, R570, N47 na nyingine.
“Mbegu hizi zinavumilia ukame, zna tija ya tani 50 hadi 130 kwa hekta, Zinastahimili magonjwa hasa ugonjwa wa fungwe, Zina mikato mingi zaidi ya minne na zina kiasi kikubwa cha sukari,” amesema.
Amesema kwa kutumia mbegu hizo, wakulima wamekuwa wakipata tija mara kwa mara kutokana na uimara wake katika mazingira mbalimbali ya kilimo.
Amesema mbegu zinazotegemea umwagiliaji hulimwa na viwanda,  nazo zina uwezo wa kutoa tija kubwa wa tani 80 hadi 200 kwa hekta, zina kiasi kikubwa cha sukari, zinavumilia magonjwa, na zina mikato zaidi ya minne.
Amesema mbegu zote huzalishwa kwa kuzingatia mfumo wa upatikanaji wa mbegu safi na salama,  hupitia hatua mbalimbali za matunzo maalum ambazo ni kuchemshwa, kutenganishwa na kukaguliwa.
Amesema zao kuu linalopatikana kwenye miwa ni sukari,  hata hivyo, katika mchakato wa uzalishaji wake, hupatikana mazao mengine kama:
molasses hutumika kama chakula cha mifugo, na tafiti zinaendelea kuhusu matumizi yake kama mbolea.
Pia Bagasse (makapi) hutumika katika uzalishaji wa umeme viwandani, briketts mkaa bora hutokana na makapi ya miwa.
Na Filter mud (mabaki) hutumika kama mbolea.
Kwa mujibu wa Mwakyusa, kila sehemu ya muwa ina faida katika mnyororo wa uzalishaji wa viwandani.
TARI Kibaha kama taasisi ya utafiti, inachangia kwa kiasi kikubwa juhudi za kupunguza pengo hilo kwa kuzalisha mbegu bora zenye tija kubwa na zinazostahimili mabadiliko ya tabianchi.
Mbegu hizo huzalishwa kwa kutumia teknolojia ya kisasa, ikiwemo njia ya kifundo ambapo ndani ya wiki sita hadi nane, mbegu tayari huwa imekomaa kwa kupandwa shambani.

You Might Also Like

Rais Samia Akabidhi Tuzo Kwa NSSF Ya Usimamizi,  Uratibu Wa Hifadhi Ya Jamii Kw Sekta Binafsi

Mpango wa Shule Salama Unaongeza ulinzi Kwa Watoto

Mgahawa unaotembea fursa kwa vijana, kutoa huduma ya unywaji wa kahawa

Kabudi Aelezea Mafanikio Ya Wizara Yake

Msomi Wa Afya, Fatuma Atia Nia Jimbo la Dodoma Mjini

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mbegu Bora za Mpunga Zazalishwa TARI Dakawa, Ifakara
Next Article Mramba Afungua Mafunzo Ya Teknolojia Ya Nishati Jua Kwa Watalaam
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Waziri Mkuu Majaliwa Akabidhi Tuzo kwa BoT Geita
Habari September 22, 2025
BoT Yarahisisha Uuzaji wa Dhahabu kwa Wachimbaji, Yatoa Punguzo La Mrabaha
Habari September 22, 2025
Waziri Mkuu Apongeza Huduma Kidijitali za NSSF, Maonesho Ya Madini Geita
Habari September 22, 2025
Mkuu Wa Mkoa Shinyanga Asifu Kazi Ya Bodi Bima Ya Amana
Habari September 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?