MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Makamu wa Rais Azindua Mpango wa Kukuza Ujuzi, Ajira kwa Vijana
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Makamu wa Rais Azindua Mpango wa Kukuza Ujuzi, Ajira kwa Vijana
Habari

Makamu wa Rais Azindua Mpango wa Kukuza Ujuzi, Ajira kwa Vijana

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
4 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: Makamu wa Rais Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema Serikali imeweka kipaumbele cha kimkakati katika kukuza ujuzi, stadi, maarifa na sifa za kuajirika au kujiajiri miongoni mwa vijana na wahitimu wa ngazi mbalimbali za elimu.
Aidha amesema, maendeleo endelevu ya Taifa hayawezekani bila kuwa na rasilimali watu iliyoelimika na yenye uwezo wa kuchangia kikamilifu katika uchumi wa Taifa.
Dkt. Nchimbi amesema hayo wakati wa uzinduzi wa mpango wa ushirikiano kati ya Taasisi za Elimu na Waajiri, uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam.
Habari Picha 11165
Ametoa wito kwa sekta binafsi kushirikiana na vyuo, kuwekeza katika tafiti hususan za sayansi na teknolojia ili kuinua viwango vya tafiti na ubora wa elimu nchini.
Kupitia mpango huo, sekta binafsi inaweza kuchangia maendeleo ya elimu kwa kufadhili tafiti na kutoa ufadhili kwa wanafunzi wa fani mbalimbali kulingana na mahitaji ya soko la ajira.
Aidha, Makamu wa Rais Dkt. Nchimbi ametoa wito kwa Taasisi za elimu na sekta binafsi kuzingatia kasi ya maendeleo ya sayansi na teknolojia duniani katika utekelezaji wa mpango huo.
Habari Picha 11166
Amesema vyuo na sekta binafsi vishirikiane kubaini ujuzi muhimu unaohitajika sasa na siku zijazo, hususan katika fani za sayansi, teknolojia, ubunifu, tiba, uhandisi na hesabu, ili kuwezesha vijana kushindana na kupata nafasi katika soko la ajira nchini na kimataifa.
Makamu wa Rais pia amesema kwamba ushirikiano baina ya taasisi za elimu na viwanda ni hitaji la lazima katika dunia ya leo, kwani vyuo haviwezi kuwa visiwa vya nadharia pekee, na viwanda haviwezi kukua bila nguvu kazi yenye ujuzi unaoendana na teknolojia na ushindani wa soko.
Habari Picha 11167
Amesema Serikali imeendelea kufanya maboresho makubwa ya sera na mitaala ya elimu katika ngazi zote, kwa lengo la kuujenga mfumo wa elimu ulio mnyumbufu, jumuishi na unaoendana na vipaji, mwelekeo na mahitaji halisi ya soko la ajira, huku ikizingatia mabadiliko ya teknolojia na ushindani wa kitaifa na kimataifa.
Uzinduzi wa mpango huo ni utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
Rais aliahidi kuanzisha mpango wa pamoja kati ya waajiri, vyuo vya ufundi stadi na vyuo vikuu, kwa lengo la kulinganisha mafunzo na mahitaji halisi ya sekta za kipaumbele za Taifa, ndani ya siku 100 baada ya kuapishwa kwake.
Habari Picha 11168
Mpango wa ushirikiano kati ya taasisi za elimu na viwanda unalenga kuimarisha uhusiano wa kimkakati kati ya utoaji wa elimu na utendaji kazi, ili kulinganisha mafunzo na mahitaji ya sekta za kipaumbele kama nishati, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), na viwanda vya kuongeza thamani.
Aidha, mpango unaweka msingi thabiti wa kujenga kizazi cha wahitimu wenye uwezo wa kuajirika, kujiajiri na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya Taifa, kwani umeelekezwa kubadilisha mfumo wa elimu ya nadharia kwenda mfumo unaozingatia ujuzi, vitendo, ubunifu na uzalishaji mali.
Uzinduzi huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Bunge, dini pamoja na wadau wa maendeleo, wakiwemo waajiri na wamiliki wa viwanda, wakuu wa taasisi mbalimbali, wakuu wa vyuo pamoja na wanafunzi.
Habari Picha 11169
Habari Picha 11170
Habari Picha 11171
Habari Picha 11172
Habari Picha 11173
Habari Picha 11174
Habari Picha 11175

You Might Also Like

Waziri Ridhiwani Awataka Wafanyakazi Kuongeza Bidii Katika Kazi

Ofisi Ya Mwandishi Mkuu Wa Sheria Yakamilisha Rasimu Ya Sheria 446 Kwa Lugha Ya Kiswahili

TARI Yaleta Mapinduzi Kilimo cha Minazi

Kasulu DC Yapongezwa Kwa Kupata Hati Safi

Kikwete: Waambieni Tunataka Maendeleo Sio Maneno

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Serikali yazindua Sera ya Taifa ya Kinga ya Jamii na ‘Hifadhi Scheme’ kwa Waliojiajiri
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Serikali yazindua Sera ya Taifa ya Kinga ya Jamii na ‘Hifadhi Scheme’ kwa Waliojiajiri
Habari February 9, 2026
CWT Yaiomba Serikali Kurekebisha Sheria za Vyama vya Wafanyakazi
Habari February 9, 2026
Serikali Yazindua Soko Kuu Jipya la Kariakoo Baada ya Moto wa 2021
Habari February 8, 2026
TALGWU Yaipongeza Timu Ya Makatibu Wa Mikoa Na Mawakili Wa Kanda Kwa Kutoa Huduma Bora Kwa Wanachama
Habari February 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?