MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mafunzo ya Usalama wa Mabwawa Kuimarisha Ulinzi wa Mazingira
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mafunzo ya Usalama wa Mabwawa Kuimarisha Ulinzi wa Mazingira
Habari

Mafunzo ya Usalama wa Mabwawa Kuimarisha Ulinzi wa Mazingira

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
WIZARA ya Maji kwa kushirikiana na taasisi binafsi imeandaa mafunzo ya usalama wa mabwawa yatakayolenga kuhakikisha miundombinu hiyo inaendelea kuwa salama kwa matumizi yaliyokusudiwa hapa nchini.
Akizungumza na vyombo vya habari katika ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Maji, Mtumba jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Rasilimali za Maji, Robert Sunday, aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, alisema mafunzo hayo yatafanyika jijini Mwanza kuanzia Oktoba 21 hadi 23, 2026.
Alitaja taasisi zinazoshirikiana na Wizara hiyo kuwa ni Chemba ya Migodi Tanzania (CMT) pamoja na Kampuni ya Uhandisi ya City, akibainisha kuwa ushirikiano huo unalenga kuimarisha uelewa wa kitaalamu kuhusu usalama wa mabwawa.
Sunday ameeleza kuwa mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo wadau na wataalamu wa mabwawa ili kuhakikisha usanifu, ujenzi na uendelezaji wa mabwawa ya maji pamoja na mabwawa ya tope sumu unazingatia viwango vinavyotakiwa.
 Amesisitiza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kulinda mazingira na vyanzo vya maji.
Washiriki wanaotarajiwa kushiriki ni kutoka serikalini na sekta binafsi, wakiwemo wamiliki wa mabwawa makubwa, wataalamu waliosajiliwa wa mabwawa pamoja na wale wanaohusika na usimamizi wa mabwawa ya maji na tope sumu.
Mafunzo hayo yataongozwa na kaulimbiu isemayo ‘Usalama wa miundombinu ya mabwawa kuanzia hatua ya usanifu, utumiaji hadi ufungaji.’
Aidha, ametumia fursa hiyo kuwaalika watunga sera, wataalamu, taasisi mbalimbali na watu binafsi wanaojishughulisha na mabwawa kujisajili kushiriki mafunzo hayo ili kuongeza ufanisi na usalama wa miundombinu hiyo muhimu.

You Might Also Like

TARURA Dar Yaendelea Na Ujenzi Wa Miundombinu Ya Barabara Iliyosimama Kutokana Na Mvua

Kingalame Aitaka Sekta Binafsi Kushirikiana na TBA Kukamilisha Mradi wa Makazi Geita

KINABO: NICHAGUENI NILETE MAJI, BARABARA KIBAMBA

Ofisi Zote Dodoma Kutoa Ushirikiano Kwa Watangazaji-RC

ICGLR Yajipanga Kujiimarisha Amani Katika Kanda

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mavunde: Makaa ya Mawe Ni Injini ya Maendeleo ya Viwanda
Next Article Serikali Yaendelea Kuimarisha Sekta Ya Utalii, Mapato Yaongezeka
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

TPHPA Yatumia Mbinu za Kibaiolojia Kudhibiti Gugu Ziwa Victoria
Habari May 24, 2026
Wizara Ya Viwanda Kutekeleza Vipaumbele Saba, Ipo  Miradi Ya Viwanda Ya  Kimkakati
Habari May 22, 2026
Biashara 15 Hazitakiwi Kufanywa Na Wageni Ndani Ya Nchi
Habari May 22, 2026
Wadau wataka mifumo jumuishi kupunguza mzigo wa malezi kwa wenye ulemavu
Habari May 21, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?