MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kusiluka aitaka TVLA kuongeza tafiti za chanjo 
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kusiluka aitaka TVLA kuongeza tafiti za chanjo 
Habari

Kusiluka aitaka TVLA kuongeza tafiti za chanjo 

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
KATIBU Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka ameitaka Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) kuongeza kasi ya kufanya tafiti za aina nyingine za Chanjo za Mifugo ambazo hazijaanza kuzalishwa ili kukidhi mahitaji ya wafugaji nchini.
Dkt. Kusiluka ameyasema hayo alipotemblea banda la TVLA akiambatana na Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Profesa Riziki Shemdoe lililopo kwenye banda jumuishi la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi (Nanenane).
“Nimefurahishwa na kazi mnayoifanya kama Wakala, endeleeni kufanya tafiti za Chanjo nyingine za magonjwa ya Mifugo ambazo hamjaanza kuzalisha ili kukinga Mifugo na magonjwa ambayo yana athari kubwa kwenye ustawi wa Mifugo nchini,” amesema.
Akitoa maelezo kuhusiana na uzalishaji wa chanjo zinazozalishwa na TVLA, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Profesa Riziki Shemdoe alisema kuwa TVLA ndio Taasisi pekee ya Serikali inayozalisha chanjo za Mifugo nchini.
Wizara imeomba fedha kwa ajili ya kuendesha kampeni ya uchanjaji mifugo nchini, Chanjo za TVLA ndio zitakazotumika kwenye zoezi hilo muhimu. Chanjo ambazo hazizalishwi na TVLA zitaagizwa kutoka kwa wazalishaji wengine,” amesema.
Aina saba za chanjo zinazozalishwa na TVLA ni pamoja na Chanjo ya Kideri au Mdondo kwa kuku (TEMEVAC), Chanjo ya Homa ya Mapafu ya Ng’ombe (CBPP), Chanjo ya Homa ya Mapafu ya Mbuzi (CCPP), Chanjo ya Kimeta (Anthrax), Chanjo ya Chambavu (Blackquarter), Chanjo ya Kimeta na Chambavu (Tecoblax) na Chanjo ya Kutupa Mimba (Brucellosis).
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka amepata maelezo kuhusina na huduma mbalimbali zinazotolewa na TVLA zikiwemo uchunguzi na utambuzi wa magonjwa ya Mifugo, Uzalishaji na Usambazaji wa Chanjo za Mifugo, Uhakiki wa ubora wa vyakula vya Mifugo, Usajili na uhakiki wa ubora wa Viuatilifu vya Mifugo, utafiti wa magonjwa ya Wanyama pamoja na huduma ya ushauri na Mafunzo.

You Might Also Like

Wakandarasi Miradi wa  TAZA Watakiwa Kukamilisha Kazi kwa Wakati 

Maadhimisho Ya VETA Ya Miaka 30 Kuhitimishwa Machi 18 Hadi 21, DSM

Tume ya Kurekebisha Sheria Yaelimisha Umma Kuhusu Haki za Wanyama

Shilingi bilioni 4.6 kupeleka umeme maeneo ya migodi

Rais Samia Azungumzia Mafanikio Ya Nishati Nchini

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Rais Mwinyi adhamiria kusimamia ubora wa bidhaa
Next Article Marekebisho ya sheria huangalia mazingira ya sasa na yajayo – Tume
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Bundi Wasaidia Kupambana na Panya: Teknolojia Asilia Inayobadili Maisha ya Wakulima
Habari August 6, 2025
Ofisa wa TARI Kuwapo Kila Kituo cha Umwagiliaji – Naibu Katibu Mkuu
Habari August 6, 2025
Mbinu Mpya za Kilimo kwa Vijana Zapata Umaarufu Nanenane Banda La VETA
Habari August 6, 2025
VETA Yatahadharisha Changamoto ya Kuzidisha Uchanganyaji wa Chakula Cha Mifugo
Habari August 6, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?