MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kasulu DC Yapongezwa Kwa Kupata Hati Safi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kasulu DC Yapongezwa Kwa Kupata Hati Safi
Habari

Kasulu DC Yapongezwa Kwa Kupata Hati Safi

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
KIGOMA: “NAWAPONGEZA Mwenyekiti wa Halmashauri, Makamu wake, Mbunge wa Kasulu Vijijini, madiwani wote, Mkurugenzi na wataalamu kwa kazi nzuri iliyowezesha halmashauri kupata hati safi katika ukaguzi wa CAG kwa mwaka ulioishia Juni 2024. Hongereni sana,”.
Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe, Kanali Michael Ngayalina ametoa pongezi hizo wakati akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Thobias Andengenye, wakati wa Mkutano Maalum wa Baraza la Madiwani kupitia na kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), uliofanyika katika Ukumbi wa Kagoma, makao makuu ya halmashauri.
Ngayalina amesema halmashauri hiyo, imepata hati safi na kupunguza idadi kubwa ya hoja hadi kufikia tarakimu moja kwa kuwa na hoja tisa kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2023/2024.
Amesema hiyo ni mara ya nne mfululizo, mafanikio ambayo yameipa  heshima si tu halmashauri hiyo, bali pia mkoa mzima wa Kigoma.
Pia amesisitiza umuhimu wa kufunga hoja zote zilizosalia kwa vielelezo na kutekeleza maagizo ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC).
Amesema lengo la mkoa ni kuhakikisha hoja zote zinapungua hadi kufikia tarakimu moja ifikapo mwaka wa fedha 2025/2026.
Naye Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Eliya Kagoma,amesema mafanikio hayo yametokana na ushirikiano mzuri baina ya madiwani, wataalamu, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, vyombo vya ulinzi na usalama, Chama Cha Mapinduzi (CCM), pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo.
Mkaguzi Mkuu wa Nje kutoka Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, Honest Muya, ameitaka halmashauri hiyo kushughulikia changamoto ya watoto kushindwa kusoma.
Ameahidi  ofisi yake kuendelea kutoa ushauri elekezi kuhusu namna bora ya kushughulikia tatizo hilo katika mwaka wa ukaguzi unaofuata.

You Might Also Like

October 2, 2024

Katibu Mkuu CCM Dkt. Nchimbi Akutana na Katibu Mkuu CRC

Spika Tulia Kufungua Kongamano La Uhuru Wa Wanataaluma Afrika UDSM

Ridhiwan Kikwete awasilisha taarifa mwenendo wa ulipaji mafao

Kamati Ya Bunge Yaridhishwa Na Utaratibu Wa Manunuzi Ya Bando

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Waandishi wa Habari wa Afrika wapata mafunzo ya Kuandika Habari za Uhamiaji
Next Article Elimu Itolewe Kuhusu Ufahamu Wa Kuwepo Kwa Fedha Maalum – Ridhiwani
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
PURA Yajipanga Gesi Asilia Itumike Kwenye Magari
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?