MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: GCLA  Yanunua Mitambo Mikubwa Inayogharimu Sh Bil 32.25 Kuimarisha Uchunguzi Wa Sampuli
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > GCLA  Yanunua Mitambo Mikubwa Inayogharimu Sh Bil 32.25 Kuimarisha Uchunguzi Wa Sampuli
Habari

GCLA  Yanunua Mitambo Mikubwa Inayogharimu Sh Bil 32.25 Kuimarisha Uchunguzi Wa Sampuli

Author
By Author
Share
2 Min Read
a Lucy Lyatuu, Dodoma
MAMLAKA ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA), imesema zaidi ya Sh bilioni 32.25 zimetumika kununua mitambo 32 mikubwa pamoja na vifaa saidizi 542, jambo ambalo limeongeza ufanisi na ubora wa uchunguzi wa sampuli mbalimbali.
Aidha imesema katika mwaka mmoja kuanzia February 2025/2026  imefanywa uchunguzi wa sampuli na vielelezo mbalimbali vipatavyo  247,286 jambo linaloongeza uelewa wa hali ya juu kwa jamii.
 Mkemia Mkuu wa Serikali,  Dk. Fidelice Mafumiko amesema hayo  wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kutangaza miradi ya maendeleo na fursa za vijana kwa mwaka 2025/2026, alisema uwekezaji huo umesaidia kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi.
Kadhalika amesema kuanzia February 2025/2026 imetengeneza ajira zaidi ya 145,000 zikiwemo za vijana wakishiriki katika  suala zima la kemikali  kwenye uingizwaii, usafirishaji pamoja na uhifadhi.
Amesema MAMLAKA imeongeza na kuimarisha  uwekezaji mkubwa katika mitambo na vifaa vya kisayansi ili kuimarisha huduma za uchunguzi wa maabara nchini.
Amesema uchunguzi unaofanywa na maabara hiyo umechangia Kwa kiwango kikubwa  Kwa jamii, kupunguza athari za dawa za kulevya kwa vijana, kuthibitisha ubora na usalama wa bidhaa za dawa asili zinazozalishwa na wataalamu wakiwemo vijana, na kutoa fursa za ajira na kujiajiri.
Aidha, ameongeza kuwa maabara hiyo inasaidia kutatua changamoto za kijamii kama kuthibitisha uhalali wa wazazi kwa watoto, kutatua migogoro ya mirathi kupitia vipimo vya DNA, na kusaidia huduma za matibabu kama kusafishwa na kupandikizwa figo, pamoja na utambuzi wa sumu kabla na baada ya kifo.
Dk. Mafumiko pia ameongeza kuwa wajasiriamali vijana wanatumia maabara hizo kupima ubora wa bidhaa zao kabla ya kuziuza sokoni, huku vyuo vikuu vinapata punguzo la asilimia 75 ya gharama za uchunguzi kwa ajili ya tafiti za kisayansi.
Aidha amesema licha ya mafanikio lakini MAMLAKA inakabiliwa na  changamoto  ikiwemo utegemezi wa wataalamu kutoka nje ya nchi katika matengenezo ya mitambo, jambo linaloongeza gharama. Ili kukabiliana na hili, Mamlaka inaendelea kuwajengea uwezo watumishi wake kufanya matengenezo hayo wenyewe.

You Might Also Like

Mwenyekiti TCCIA Geita Gabriel Ahamasisha Watanzania Kutumia Bidhaa Za Ndani

Elimu Ya Afya, Takwimu sahihi Na Ufuatiliaji Ni Muhimu Kuimarisha Huduma Za Chanjo

BRELA kuanza kuwasajili wakulima

Dkt. Mashimba Achukua Fomu Ya Kuwania Nafasi Ya Ubunge

Ridhiwani Awashika Mkono Wenye Mahitaji Maalum

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TPDC Kufikisha Gesi Nchi Nzima  Ndani Ya Miaka Miwili Na Nusu  Kuanzia Sasa
Next Article Ofisi Ya Taifa Ya Takwimu  Kufanya Tafiti Kwa Wakala Wa Huduma Za Fedha,Viwandani
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vita Mashariki ya Kati Vyatikisa Uchumi wa SADC, Mawaziri Watakiwa Kuchukua Hatua
Habari March 12, 2026
Mamlaka Za Mitaa Ondoeni Urasimu Katika Kuanzisha Biashara Mpya-Waziri Mkuu
Habari March 12, 2026
Ofisi Ya Taifa Ya Takwimu  Kufanya Tafiti Kwa Wakala Wa Huduma Za Fedha,Viwandani
Habari March 12, 2026
TPDC Kufikisha Gesi Nchi Nzima  Ndani Ya Miaka Miwili Na Nusu  Kuanzia Sasa
Habari March 11, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?