MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: FAJ Yataka Wahamiaji Wa Kazi Wa Afrka, Wanaokwenda Maeneo Mengine Walindwe
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > FAJ Yataka Wahamiaji Wa Kazi Wa Afrka, Wanaokwenda Maeneo Mengine Walindwe
Habari

FAJ Yataka Wahamiaji Wa Kazi Wa Afrka, Wanaokwenda Maeneo Mengine Walindwe

Author
By Author
Share
4 Min Read
Na Lucy Ngowi
KENYA: WAANDISHI wa Habari Afrika wametakiwa kuandika matatizo wanayokutana nayo wahamiaji wa kazi wa bara hilo wanapokwenda nchi nyingine  ili kuyafichua hatua stahiki zichukuliwe.
Rais wa Shirikisho la Waandishi wa Habari Afrika (FAJ), Omar Faruk Osman amesema hayo wakati wa mafunzo  ya siku tatu yaliyoandaliwa Chini ya Mpango wa pamoja wa Uhamiaji wa Wafanyakazi (JLMP), kwa ushirikiano na Tume ya Umoja wa Afrika (IOM).
Shirika la Kazi Duniani (ILO) na Shirikisho la Waandishi wa Habari Afrika (FAJ).
Osman amesema kwa sababu hiyo, ni vema kutoruhusu habari na historia za Afrika zielezwe na watu wengine kwa namna wanavyotaka wao.
“Hatuwezi kuunda wala kuelezea simulizi ya bara letu au watu wetu ikiwa hatuandiki sisi wenyewe. Mwisho wa siku, uandishi wa habari ni huduma kwa jamii.
“Kama hatuwezi kuwatumikia watu wetu, kama hatuwezi kueleza historia yao kwa namna wanayotaka au inayoakisi uhalisia wao, basi hatufanyi uandishi wa habari kwa ajili ya jamii.
“Tunakuwa kama mashine ya kusambaza taarifa zilizotumwa. Tunachapisha na kukimbiza habari hizo. Lakini historia ya kibinadamu, namna watu wetu wanavyoteseka, namna wanavyodhalilishwa, ni jambo lililo karibu sana nasi—na lazima tufanye jambo kuhusu hilo,” amesema.
Amesema amefurahi kuona kuna ajenda ya vyombo vya habari kuhusu uhamiaji.
“Tunapaswa kutumia fursa hii kueleza historia ya watu wetu, kuonesha mateso ya ndugu zetu wanaorejea wakiwa kwenye majeneza.
“Angalia yanayofanyika katika nchi za Ghuba—ni ya aibu sana. Nchi hizo zinajitajirisha kupitia wafanyakazi wahamiaji. Lakini watu wetu, je, wanatajirika? Hapana. Je, afya zao na ustawi wao vinazingatiwa? Hapana.
“Je, wanakabiliwa na unyanyasaji mkubwa? Ndio. Je, tunasema chochote? Hapana,” amehoji Osman.
Amesema Afrika ina sheria, sera na kanuni nyingi lakini tatizo kubwa lililopo ni utekelezaji wake.
“Wanasiasa wetu, kuanzia wabunge, hawatekelezi kile kinachopaswa kufanyika. Na kwa kuwa hatufanyi hivyo, hatupaswi kuendelea kuzalisha sera mpya kila wakati.
“Tunahitaji kujikita katika kuhakikisha kuwa watu wetu wanalindwa. Na njia pekee ni kufichua madhila hayo.
“Sijui ni wangapi kati yenu mnajua kuwa wiki iliyopita kule Geneva, vyama vya wafanyakazi vya Afrika viliwasilisha malalamiko rasmi dhidi ya Saudi Arabia.
“Ilikuwa malalamiko makubwa na yenye uzito mkubwa zaidi kuwahi kufikishwa kwa ILO dhidi ya nchi hiyo. Watu walidharau—walidhani Waafrika hawawezi kufanya hivyo,” amesema.
Amesema pamoja na kutolewa kwa hoja hiyo vyombo vya habari vya Afrika viliripoti kwa uchache.
“Ukienda uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta kila siku, utaona dada na kaka zetu wakirudi kwa machozi, na si lazima wawe kwenye majeneza.
“Je, tunasimuliaje simulizi hiyo? Ina sura ya kibinadamu yenye kugusa sana. Je, tunawaambiaje Umoja wa Afrika wahakikishe kuwa nchi wanachama wanatekeleza yale waliyoafikiana?
“Je, tunawafichuaje wanasiasa wala rushwa wanaoshirikiana na Waarabu matajiri wanaofadhili serikali zetu ili kuficha madhila haya? Je, tunainuaje hadhi ya Waafrika? Je, tunasemaje kuwa “maisha ya watu weusi ni muhimu” kwa njia yetu sisi wenyewe? Hili ni muhimu sana,” amehoji.
Amesema waandishi wa habari wanapaswa kuzungumza kwa niaba ya waafrika, kuwapa sauti, kueleza historia yao na kuifichua wanayotendewa.

You Might Also Like

TANESCO Tunathamini Wadau Wa Maendeleo- Nyamo-Hanga

Trilioni 1.3  Zatumika Kuboresha Afya Ya Msingi Nchini

SEforALL Kuimarisha Ushirikiano Upatikanaji Nishati Endelevu

Kanisa La GCC Kufanya Maombi Kuelekea Uchaguzi Mkuu

TRAWU Kupambania Mkataba Wa Hali Bora Kwa Wafanyakazi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Elimu Itolewe Kuhusu Ufahamu Wa Kuwepo Kwa Fedha Maalum – Ridhiwani
Next Article Serikali Yatumia Zaidi Ya Bilioni 100 Kupeleka Umeme Simiyu
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mramba Afungua Mafunzo Ya Teknolojia Ya Nishati Jua Kwa Watalaam
Habari August 7, 2025
Mbegu Bora za Miwa Zenye Tija ya Tani 200 kwa Hekta Zaendelea Kuwanufaisha Wakulima
Habari August 7, 2025
Mbegu Bora za Mpunga Zazalishwa TARI Dakawa, Ifakara
Habari August 7, 2025
Mtego wa Inzi Wa Matunda Suluhisho Salama kwa Wakulima
Habari August 7, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?